Hamia kwenye habari

Ndugu Boris Simonenko na mke wake, Ida

FEBRUARI 1, 2023 | HABARI ZIMEONGOZWA: AGOSTI 1, 2023
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AHUKUMIWA | “Hali Zangu Hazihitaji Kubadilika”

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU AHUKUMIWA | “Hali Zangu Hazihitaji Kubadilika”

Mahakama ya Jiji la Kovrovskiy iliyo katika Eneo la Vladimir ilimhukumu Ndugu Boris Simonenko kifungo cha miaka miwili na miezi saba gerezani. Hata hivyo, kwa sababu ya muda ambao amekuwa mahabusu na katika kifungo cha nyumbani, anahesabiwa kuwa kifungo chake kimekwisha. Hahitaji kwenda gerezani wakati huu.

Maelezo Mafupi Kumhusu

Tuna uhakika kwamba Boris na familia yake watapata nguvu na shangwe wanapoendelea kubaki karibu na Yehova.​—1 Mambo ya Nyakati 16:27.

Mfuatano wa Matukio

  1. Februari 8, 2021

    Wenye mamlaka walirekodi mazungumzo kupitia vinasa-sauti na kutumia rekodi hizo kuanzisha rasmi uchunguzi

  2. Februari 17, 2021

    Nyumba yao ilifanyiwa msako. Alihojiwa na kuwekwa kizuizini

  3. Februari 18, 2021

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa. Alishtakiwa kwa kuongoza mikutano ya Mashahidi wa Yehova kupitia Intaneti. Aliwekwa mahabusu

  4. Julai 13, 2021

    Aliachiliwa kutoka mahabusu na kuwekwa kwenye kifungo cha nyumbani

  5. Februari 17, 2022

    Aliachiliwa kutoka kwenye kifungo cha nyumbani na kuwekewa vizuizi vya kusafiri

  6. Septemba 15, 2022

    Kesi ya uhalifu ilianza