Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Umoja Ulimwenguni Pote Si Ndoto Tu

Umoja Ulimwenguni Pote Si Ndoto Tu

Umoja Ulimwenguni Pote Si Ndoto Tu

Mtu mmoja katika jimbo la Kerala nchini India aliwaandikia hivi wachapishaji wa gazeti hili: “Gazeti lenu la Amkeni! halina kifani. Ninaamini kwamba gazeti hili limezungumzia karibu mambo yote. Nimefurahia kusoma makala zinazozungumza hasa kuhusu mambo ya asili.”

Mwanamume huyo alivutiwa na gazeti la Amkeni! kwa sababu moja hususa. Alieleza hivi: “Sidhani kuna gazeti jingine ambalo linaweza kuwasaidia watu wa mataifa mbalimbali kuwa kama ndugu kama gazeti la Amkeni! Hakuna gazeti jingine linaloendeleza wazo la umoja wa ulimwenguni pote kama gazeti la Amkeni! Kwa kulinganisha magazeti mengi ninayosoma, ninaweza kusema kwamba Amkeni! ni gazeti lenye thamani.”

Maoni ya msomaji huyo kuhusu gazeti la Amkeni! yanapatana na kusudi lake linaloonyeshwa kwenye ukurasa wa 4 wa kila toleo, yaani: “Linabaki sikuzote bila kuingilia siasa wala kutukuza jamii moja ya watu juu ya nyingine.” La maana kuliko yote, gazeti la Amkeni! huwaelekeza wasomaji kwa Muumba wetu ili wapate majibu kwa maswali muhimu ya maisha.

Broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? yenye kurasa 32 hufanya hivyo pia. Miongoni mwa masomo yake 16 kuna yale yenye vichwa kama “Mungu Ni Nani?,” “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?,” na “Ufalme wa Mungu Ni Nini?” Waweza kuomba nakala ya broshua hiyo kwa kujaza kuponi iliyo hapa na kuituma kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Nitumieni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Onyesha lugha unayotaka.

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.