Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Anajivunia Baba Yake

Anajivunia Baba Yake

Anajivunia Baba Yake

‘SASA ninajivunia baba yangu hata zaidi!,’ ndivyo msichana mwenye umri wa miaka 12 alivyoandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini India. Alirejezea kichwa “Baba Wanaopendezwa Wanakuwa na Wana Wenye Furaha” katika sehemu ya “Kuutazama Ulimwengu” ya toleo la Amkeni! la Agosti 22, 1999. Sehemu hiyo ilizungumzia uchunguzi mmoja ulioonyesha kwamba wana watakuwa watu wazima wanaojiamini na wenye mtazamo unaofaa, iwapo baba zao watatumia wakati pamoja nao na kuwajali.

Msichana huyo alisema kwamba yeye na dada yake pacha wamebarikiwa kwa sababu baba yao anawajali sana. Alisema kwamba anafurahia kusoma kuhusu matukio ya ulimwengu katika Amkeni!, na aliendelea kusema kwamba “gazeti hili lafaa wanafunzi wa siku hizi.”

Ili kusaidia familia mbalimbali kushughulikia matatizo yanayokumba wanadamu leo, Mashahidi wa Yehova wamechapisha kitabu chenye kurasa 192 kinachoitwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kitabu hicho kina mwongozo mzuri kwa kila mtu katika familia—waume, wake, wazazi, watoto na babu na nyanya. Baadhi ya sura zake zenye ushauri mzuri ni “Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana,” “Saidia Tineja Wako Asitawi,” “Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu,” na “Dumisha Amani Nyumbani Mwako.”

Waweza kupokea kitabu hicho kwa kujaza na kutuma kuponi iliyopo hapa kwenye anwani iliyoonyeshwa au kwenye anwani ifaayo iliyoorodhesha katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili. Utafaidika kwa kupata madokezo yanayoweza kukusaidia kutatua matatizo na kufanya maisha yako ya familia yawe yenye furaha jinsi Muumba alivyokusudia.

□ Nitumieni kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.