Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Alitetea Imani Yake

Alitetea Imani Yake

Alitetea Imani Yake

▪ Hivi karibuni wakati wa likizo, Morgan, mwenye umri wa miaka saba aliye katika darasa la kwanza alipewa mgawo wa kusoma hadithi kuhusu Krismasi. Morgan alimkumbusha mwalimu wake kwamba alihisi sherehe hiyo haipatani na Biblia. Mwalimu wake alimruhusu achague hadithi ambayo haitasumbua dhamiri yake.

Muda fulani baadaye, kulikuwa na sherehe ya kutoa zawadi katika shule hiyo na familia ya Morgan ilialikwa. Morgan alishangaa alipopewa zawadi kwa ajili ya ujasiri wake wa kutetea imani yake. Alipoulizwa jinsi alivyositawisha ujasiri kama huo, alieleza kwamba yeye na familia yake walisoma pamoja kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, kinachozungumzia mambo yanayohusu maisha na mafundisho ya Yesu Kristo.

Kitabu hicho chenye kurasa 256, kilicho na picha nyingi zenye kupendeza, kinaweza kuwasaidia wazazi kuwa na mazungumzo yenye kufurahisha pamoja na watoto wao. Kina sura kama vile “Kwa Nini Hatupaswi Kusema Uwongo?,” “Je, Karamu Zote Zinampendeza Mungu?,” na “Jinsi Tunavyoweza Kuushinda Woga.”

Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini, na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.