Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutafuta Wakati kwa Ajili ya Mambo Muhimu

Kutafuta Wakati kwa Ajili ya Mambo Muhimu

Kutafuta Wakati kwa Ajili ya Mambo Muhimu

“Wakati uliobaki umepungua.”—1 Wakorintho 7:29.

“KURUKARUKA na kupigapiga maji hakumaanishi unajua kuogelea,” akaandika Michael LeBoeuf katika kitabu chake Working Smart.

Kwa maneno mengine, kuna tofauti kati ya kutimiza jambo na kulifanya tu. Fikiria utendaji wako wa juma lililopita. Ulitenga wakati wako ili ufanye nini? Ni nini ambacho hukuweza kufanya kwa kuwa ulikuwa na shughuli nyingi? Je, unaona uhitaji wa kutenga wakati zaidi kufanya mambo unayoona kuwa muhimu zaidi?

Fikiria yale ambayo Yesu alitabiri kuhusu nyakati zetu zenye shughuli nyingi. Alisema kwamba wanafunzi wake wangekuwa na shughuli nyingi mwisho wa mfumo huu unapokaribia na kufuatiwa na ulimwengu mpya wa Mungu. Wangekuwa wakifanya nini? Wakihubiri “habari njema ya ufalme” wa Mungu. Yesu pia alisema kwamba watu wengi wangekuwa na shughuli nyingi sana hivi kwamba hawangesikiliza ujumbe huo. Wangekuwa wakijishughulisha sana na mambo ya kawaida ya maisha. Aliongeza kwamba wale ambao wangekuwa na shughuli nyingi sana hivi kwamba wasiwe na wakati wa kusikiliza ujumbe wa Ufalme wangeharibiwa.—Mathayo 24:14, 37-39; Luka 17:28-30.

Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu katika nchi zaidi ya 230. Kama Yesu alivyotabiri, watu wengi hawataki kuwasikiliza kwa hiyo wanatoa udhuru wa kwamba wana shughuli nyingi. Tunakukaribisha utenge wakati ili uchunguze kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu Ufalme wa Mungu. Tunatumaini kwamba baada ya kujifunza kuhusu baraka ambazo Mungu amewaahidi wanadamu, utakubali kwamba kusikiliza na kutii ujumbe wa Biblia ni jambo la maana sana, jambo unalostahili kutenga wakati ili ufanye. *

[Maelezo]

^ fu. 6 Ili ujifunze zaidi, wasiliana na Mashahidi wa Yehova wa kwenu au uandike barua kwa kutumia anwani inayofaa kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 au utumie kituo cha Intaneti www.watchtower.org.