Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kaa Karibu na Yehova!”

“Kaa Karibu na Yehova!”

“Kaa Karibu na Yehova!”

Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova

● Maelfu ya makusanyiko haya ya siku tatu, ambao yamepangiwa kuanzia Marekani kwenye mwisho juma wa Mei 21-23 (Mwezi wa 5), yatafanywa ulimwenguni pote kwa miezi kadhaa itakayofuata. Kila siku vipindi vitaanza kwa programu ya muziki saa 3:20 asubuhi. Kichwa kikuu cha Ijumaa (Siku ya 5) kinachotegemea andiko la Zaburi 73:28 ni “Kumkaribia Mungu Ni Kwema Kwangu.” Hotuba ya mwenyekiti itafuatwa na hotuba yenye kichwa “Makusanyiko Hutusaidia Kukaa Karibu na Yehova” na “Mwana Anapenda Kumfunua.” Kisha mfululizo wenye kichwa “Igeni Wale Waliodumisha Uhusiano wa Karibu na Yehova” utazungumzia jinsi Abrahamu, Ruthu, Hezekia, na Maria walivyofanya hivyo. Programu ya asubuhi itamalizika kwa hotuba ya msingi yenye kichwa “Jinsi Yehova Anavyotukaribia.”

Sehemu ya kwanza ya Ijumaa alasiri ina kichwa “Majibu ya Maswali Kumhusu Yehova,” itafuatwa na hotuba yenye kichwa “Ruhusu Nidhamu ya Yehova Ikufinyange” na “Usiwe na ‘Ghadhabu Juu ya Yehova.’” Kisha kutakuwa na mfululizo wenye sehemu tano wenye kichwa “Mawasiliano Husaidia Familia Kukaa Karibu na Yehova.” Sehemu hizo zitakuwa na vichwa vifuatavyo: “Yehova Ndiye Mwasiliani Mkuu,” “Waume, Wasilianeni na Wake Zenu!,” “Wake, Wasilianeni na Waume Wenu!,” “Wazazi, Wasilianeni na Watoto Wenu!,” na “Watoto, Wasilianeni na Wazazi Wenu!” Kipindi cha alasiri kitamalizika kwa hotuba “Uumbaji Unamfunua ‘Mungu Aliye Hai’!”

Kichwa kikuu Jumamosi (Siku ya Posho) ni “Urafiki Wake Uko Pamoja na Watu Wanyoofu,” kinachotegemea Methali 3:32. Mfululizo wenye sehemu tano “Wasaidie Watu ‘Wapatanishwe na Mungu’” utakuwa na hotuba zenye kichwa “Waliotenganishwa, Wasio na Tumaini,” “Naye Akawauliza Maswali,” “Timiza Mgawo Wako Ukiwa Mfanyakazi Mwenzi Katika Kueneza Injili,” “Wavuteni Kupitia Mwenendo Mzuri,” na “Endelea Kujitahidi kwa Bidii.” Baada ya hotuba yenye kichwa “Utumishi wa Wakati Wote Unaimarisha Uhusiano Wako Pamoja na Yehova” na “Wale Wanaompenda Yehova Hawana Kitu cha Kuwakwaza,” kipindi hicho kitamalizika kwa hotuba ya ubatizo, na baada ya hapo wale wanaostahili watabatizwa.

Programu ya Jumamosi alasiri itakuwa na mfululizo wenye sehemu nane wenye kichwa, “Usiruhusu Kitu Chochote Kikutenganishe na Yehova”—“Mbinu za Shetani Zisizo za Wazi,” “Kiburi,” “Pesa,” “Afya,” “Kazi,” “Tafrija,” “Familia,” na “Teknolojia.” Itafuatiwa na drama ya pekee ya sauti yenye kichwa “Usife Moyo Unaporekebishwa na Yehova!” Hotuba ya mwisho ya siku hiyo itakuwa na kichwa “Kaa Karibu na Yehova, Kama Yeremia Alivyofanya.”

Kichwa kikuu cha Jumapili (Siku ya Yenga) kinachotegemea Yoshua 23:8 ni “Yehova . . . Ndiye Mnayepaswa Kushikamana Naye.” Baada ya wimbo na sala ya asubuhi, mfululizo wenye kichwa “Kuthamini Sifa za Yehova Zenye Kuvutia” utazungumzia kila moja ya sifa hizi nane—“Mwenye Kufikika,” “Hisia-Mwenzi,” “Uthamini,” “Mkarimu,” “Kutobagua,” “Kusamehe,” “Usawaziko,” na “Ushikamanifu.” Hotuba ya watu wote yenye kichwa “Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?” itafuata. Kipindi cha asubuhi kitamalizika kwa muhtasari wa Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma.

Sehemu ya pekee ya Jumapili alasiri ni drama yenye waigizaji yenye kichwa “Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona.” Itazungumzia jinsi Wakristo wa karne ya kwanza walivyokimbia kutoka Yerusalemu. Baada ya drama hiyo, kusanyiko litamalizika kwa hotuba yenye kichwa “Kaa ‘Mahali pa Siri pa Aliye Juu Zaidi.’”

Fanya mipango sasa ili uhudhurie. Ili upate habari kuhusu kusanyiko ambalo litafanywa karibu nawe, tembelea Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililo karibu nawe au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili. Gazeti la Machi 1 la Mnara wa Mlinzi, linalotolewa pamoja na gazeti hili, pamoja na tovuti ya www.ps8318.com ina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yatafanyiwa.