Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MNARA WA MLINZI Na. 1 2018 | Biblia—Kitabu Kisichopitwa na Wakati!

BIBLIA—KITABU KISICHOPITWA NA WAKATI!

Je, ushauri wa Biblia umepitwa na wakati, hasa ukifikiria jinsi ilivyo rahisi leo kupata habari kwa uharaka kutokana na maendeleo makubwa ya teknolojia? Biblia inasema:

“Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida.”—2 Timotheo 3:16.

Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linachanganua madai ya Biblia kwamba inaweza kutuongoza katika kila nyanja ya maisha yetu.

 

Je, Ushauri wa Biblia Unaweza Kutumika Leo?

Kwa nini utafute ushauri wa kitabu kilichokamilishwa miaka 2,000 hivi iliyopita, ilhali unaweza kupata ushauri unaotegemea habari za karibuni zaidi?

Mafundisho ya Biblia​—Hekima Isiyopitwa na Wakati

Biblia haijapitwa na wakati. Badala yake, ina mafundisho yanayotegemea kanuni na viwango ambavyo vinatufaa leo na vyenye kudumu

Imepitwa Ama Ipo Mbele ya Wakati?

Biblia si kitabu cha sayansi, lakini inataja mambo ya kisayansi ambayo huenda yakakushangaza.

1 Hutusaidia Kuepuka Matatizo

Chunguza jinsi ambavyo hekima ya Mungu imewasaidia watu kuepuka baadhi ya matatizo mazito sana maishani.

2 Hutusaidia Kutatua Matatizo

Biblia ina hekima inayoweza kutusaidia kutatua matatizo ambayo yametusumbua kwa muda mrefu kama vile, wasiwasi wa kupita kiasi, kuahirisha mambo, na upweke.

3 Hutusaidia Kuvumilia Matatizo

Namna gani kuhusu matatizo ambayo hatuwezi kuyaepuka wala kuyatatua, kama vile ugonjwa wa kudumu au kufiwa?

Biblia na Wakati Wako Ujao

Neno la Mungu linaweza kutusaidia kushughulika na kile kilicho karibu yetu, yaani, matatizo ya kila siku tunayokabili katika ulimwengu huu usiotabirika. Lakini zaidi ya hilo, Biblia huangazia pia wakati wetu ujao.

Una Maoni Gani?

Ona mambo ambayo baadhi ya watu wanaamini na kile ambacho Biblia inafundisha kuhusiana na swali hili.