Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kujulisha Jina la Yehova”

“Kujulisha Jina la Yehova”

“Kujulisha Jina la Yehova”

MAGAZETI Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanathaminiwa ulimwenguni pote kwa sababu ya habari za kiroho na zenye kuelimisha. Msomaji mmoja nchini Ufaransa anaonyesha uthamini huo katika barua ifuatayo aliyoiandika hivi majuzi:

“Mimi ni mwanamke kijana, mzaliwa wa Afrika na sijasoma sana. Hivi majuzi nilianza kusoma magazeti yenu. Kwa kuvutiwa na habari zake, nimegundua umuhimu wa kusoma. Kupitia magazeti yenu, nimeboresha msamiati wangu na ninaweza kuandika barua isiyo na makosa mengi.

“Ninashangaa kuona kwamba mnazungumzia kila jambo linalohusu wanadamu, sayari, na Muumba. Makala hizi zinaeleweka kwa urahisi sana hivi kwamba humchochea mtu awe msomaji mwenye bidii. Hakuna mtu mwingine yeyote aliye na uwezo wa kufundisha watu wa aina zote kwa wakati uleule.

“Pia mimi hushangaa kuona kwamba kazi hii yote haifanywi ili kupata faida bali ili kujulisha jina la Yehova. Ninajua kwamba mna kibali chake, nami nawashukuru. Tafadhali endeleeni kumtegemea Muumba awape nguvu ili mfundishe.”

Kwa sasa, Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi yao ya kufundisha watu Biblia katika nchi 235. Gazeti Mnara wa Mlinzi linachapishwa katika lugha 148 nalo Amkeni! katika lugha 87. Magazeti hayo hayachapishwi ili kumpa sifa mwanadamu yeyote. Shauri linalotegemea Biblia pamoja na habari ya kisasa inayopatikana katika magazeti hayo zimekusudiwa kumtukuza Muumba anayesema: ‘Mimi, Yehova, Ndiye ninayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe.’ (Isaya 48:17) Na unufaike kwa kusoma Maandiko Matakatifu kwa ukawaida kwa kutumia vifaa hivyo vya kujifunzia Biblia.