MNARA WA MLINZI—TOLEO LA FUNZO Februari 2015

Toleo hili lina makala za funzo za Aprili 6 hadi Mei 3, 2015.

Wajapani Wapokea Zawadi Ambayo Hawakutarajia

Kitabu kipya kinachoitwa “Biblia—Injili ya Mathayo” kilitolewa nchini Japani. Kina mambo gani? Kwa nini kilitayarishwa?

Iga Unyenyekevu na Wororo wa Yesu

Andiko la 1 Petro 2:21 linatuagiza tufuate hatua za Yesu kwa ukaribu. Ingawa sisi ni wanadamu wasio wakamilifu, tunawezaje kuiga unyenyekevu na wororo wa Yesu?

Iga Ujasiri na Utambuzi wa Yesu

Kupitia yale ambayo yameandikwa katika Biblia, tunajifunza utu wa Yesu. Ona jinsi tunavyoweza kufuata hatua zake kwa ukaribu kwa kuiga ujasiri na utambuzi wake.

Dumisha Bidii Yako Katika Huduma

Tunajua kwamba kuhubiri habari njema ndiyo kazi muhimu zaidi tunayoweza kufanya leo. Tunawezaje kuongeza na hata kudumisha bidii yetu katika huduma ya Kikristo?

Kutayarisha Mataifa kwa Ajili ya “Fundisho la Yehova”

Wakristo wa mapema walifanikiwa kadiri gani kuhubiri habari njema? Ni nini ambacho huenda kilirahisisha kazi ya kuhubiri katika karne ya kwanza kuliko wakati mwingine wowote katika historia?

Yehova Huongoza Kazi Yetu ya Kufundisha Ulimwenguni Pote

Ni mambo gani ambayo yametukia katika nyakati za karibuni ambayo yamewawezesha watumishi wa Yehova kuhubiri habari njema kwa mafanikio duniani pote?

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Tunaweza kufanya nini ili kuwasaidia ndugu na dada wanaoathiriwa na marashi? Ni katika hali gani mhubiri wa Ufalme mwanamke anahitaji kufunika kichwa?

HIFADHI YETU YA VITU VYA KALE

“Majira Muhimu Sana”

Zion’s Watch Tower liliita wakati wa Ukumbusho wa Kifo cha Kristo ‘majira muhimu sana’ na liliwahimiza wasomaji waadhimishe. Ukumbusho uliadhimishwaje katika siku za mapema?