Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Mwisho utakapofika, ni baadhi ya mambo gani yataondolewa?

Baadhi ya mambo yatakayoondolewa ni serikali za wanadamu, vita na ukosefu wa haki, dini ambazo hazimpendezi Mungu wala kuwasaidia wanadamu, na watu wasiomwogopa Mungu.—5/1, ukurasa wa 3-5.

Gogu wa Magogu anayetajwa katika kitabu cha Ezekieli ni nani?

Inaonekana kwamba Gogu wa Magogu si Shetani, bali ni muungano wa mataifa yatakayojaribu kuwaangamiza watu wa Mungu baada ya dhiki kuu kuanza.—5/15, ukurasa wa 29-30.

Ni mambo gani sita yanayoweza kumsaidia mtu akabiliane vizuri na uzee?

Biblia inashauri mtu awe na sifa zifuatazo: (1) kiasi, (2) usawaziko, (3) mtazamo unaofaa, (4) ukarimu, (5) mwenye urafiki, na (6) mwenye shukrani. Sifa hizo zinaweza kumsaidia mtu akabiliane vizuri na uzee.—6/1, ukurasa wa 8-10.

Miujiza ya Yesu inaonyeshaje kwamba alikuwa mkarimu?

Katika karamu ya harusi huko Kana, Yesu alibadili lita 380 za maji kuwa divai. Isitoshe, wakati fulani aliwalisha kimuujiza watu zaidi ya 5,000. (Mt. 14:14-21; Yoh. 2:6-11) Katika visa vyote, Yesu alikuwa akiiga ukarimu wa Baba yake.—6/15, ukurasa wa 4-5.

Ingawa sisi si wakamilifu, kwa nini tuna uhakika kwamba tunaweza kumpendeza Mungu?

Wanaume kama vile Ayubu, Loti, na Daudi walifanya makosa. Hata hivyo, walitaka kumtumikia Yehova, walitubu makosa yao, na wakabadili njia zao. Walipata kibali cha Yehova; sisi pia tunaweza kufanya kama wao.—7/1, ukurasa wa 12-13.

Je, washiriki wote wa dini za uwongo watauawa Babiloni Mkubwa anapoharibiwa?

Inaonekana sivyo. Andiko la Zekaria 13:4-6 linaonyesha kwamba hata baadhi ya viongozi wa kidini wataacha dini zao na kusema kwamba hawakuwahi kushirikiana nazo.—7/15, ukurasa wa 15-16.

Kwa nini Baraka alisema kwamba angekubali kupigana vita ikiwa tu Debora angekubali kuandamana naye?

Baraka alikuwa mwanaume mwenye imani. Badala ya kumwomba Yehova silaha zaidi, alitaka kuandamana na mwakilishi wa Mungu—Debora—ili amwimarishe yeye na watu wake. (Amu. 4:6-8; 5:7)—8/1, ukurasa wa 13.

Mkristo anapaswa kutafakari mambo gani?

Baadhi ya mambo hayo ni uumbaji wa Yehova, Neno lake lenye thamani, zawadi ya sala, na zawadi ya fidia.—8/15, ukurasa wa 10-13.

Kuepuka mashirika mabaya kunatusaidiaje tunapotaka kuanzisha urafiki wa kimapenzi?

Tunawatendea kwa fadhili watu ambao hawamwabudu Yehova. Hata hivyo, kuanzisha urafiki wa kimapenzi na mtu ambaye hajajiweka wakfu na si mwaminifu kwa Yehova ni kukiuka mwongozo Wake. (1 Kor. 15:33)—8/15, ukurasa wa 25.

Imani ya Petro ilidhoofika jinsi gani, na ni nini kilichomsaidia kuwa tena na imani thabiti?

Kwa imani, Petro alitembea juu ya maji na kumfuata Yesu. (Mt. 14:24-32) Lakini alipotazama dhoruba, Petro aliogopa. Kisha akamkazia tena fikira Yesu na kukubali msaada wake.—9/15, ukurasa wa 16-17.

Andiko la Matendo 28:4 linasema kwamba watu wa Malta walifikiri kwamba mtume Paulo alikuwa muuaji. Kwa nini walifikiri hivyo?

Nyoka kipiri alipomuuma Paulo, huenda walikata shauri kimakosa kwamba alikuwa akiadhibiwa na Mungu wa kike wa haki anayeitwa Dike.—10/1, ukurasa wa 9.

Kisa cha Martha cha kukengeushwa na shughuli nyingi kinatufundisha nini?

Wakati fulani Martha alikengeuka kwa sababu alitaka kutayarisha mlo wa pekee. Yesu alisema kwamba Maria alichagua fungu jema alipoamua kusikiliza mafundisho yake. Tunahitaji kuwa makini ili mambo yasiyo ya lazima yasivuruge shughuli za kiroho.—10/15, ukurasa wa 18-20.