Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Kristo aliwaambia wafuasi wake kwamba alikuja duniani, “si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa nafsi yake kuwa fidia badala ya wengi.” (Mathayo 20:28) Alitoa uhai wake kwa kupenda ili kuwafaidi wengine.

Yesu alitoa jinsi gani fidia au dhabihu ya ukombozi kupitia kifo chake? Kwa nini dhabihu hiyo ilihitajiwa? Yesu alitoa uhai wake kwa ajili ya nani? Na kifo chake kinaweza kuwa na maana gani kwako?

Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ukusanyike pamoja nao ili uchunguze majibu ya Biblia kwa maswali hayo. Mwaka huu, ukumbusho wa kifo cha Yesu utakuwa Jumanne, Machi (Mwezi wa 3), tarehe 30, baada ya jua kushuka. Wakati huo, maswali yaliyo hapo juu yatajibiwa kwa kutumia Maandiko.

Unaweza kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu. Waulize Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe kuhusu saa hususa na mahali pa kukutania.