Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mtu Mwenye Ukoma Aponywa!

Mtu Mwenye Ukoma Aponywa!

Kwa Ajili ya Vijana

Mtu Mwenye Ukoma Aponywa!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Naamani, Elisha, na msichana Mwisraeli ambaye hajatajwa jina.

Muhtasari: Naamani, mkuu wa jeshi la Siria anaponywa ugonjwa mbaya baada ya msichana Mwisraeli kumshauri akamwone Elisha.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA 2 WAFALME 5:1-19.

Unafikiri msichana huyo mdogo alilazimika kukabiliana na hisia gani, ukizingatia kwamba alikuwa ametekwa kutoka katika familia yenye kumwogopa Mungu?

․․․․․

Je, unaweza kuwazia jinsi Naamani, mwanamume hodari, alivyokatishwa tamaa na ugonjwa wake wenye kudhoofisha?

․․․․․

Unatambua hisia gani katika mazungumzo ya Naamani na watumishi wake kwenye mstari wa 11 mpaka wa 13?

․․․․․

Kuanzia mstari wa 15, unatambua badiliko gani la mtazamo kwa upande wa Naamani?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Ni mambo gani ambayo huenda yalimfanya Naamani awe na kiburi? (Soma tena mstari wa 1.)

․․․․․

Kwa kutumia vifaa vya utafiti unavyoweza kupata, chunguza kuhusu ukoma nyakati za Biblia. * (Kwa mfano, ugonjwa huo ulikuwa mbaya kiasi gani? Je, ulikuwa ugonjwa wa kuambukiza? Ulitibiwa jinsi gani?)

․․․․․

Unafikiri kuponywa kwa Naamani kulikuwa na matokeo gani juu ya msichana mdogo Mwisraeli?

․․․․․

Huenda jibu la Elisha lilimtia Naamani kwenye jaribu katika njia gani? (Ona mstari 10.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Hatari za kuwa mwenye kiburi.

․․․․․

Ujasiri unapozungumza kuhusu imani yako.

․․․․․

Nguvu za Yehova za kuponya magonjwa.

․․․․․

4 NI JAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBALO LIMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

IKIWA HUNA BIBLIA, WAOMBE MASHAHIDI WA YEHOVA WAKUPE MOJA, AU SOMA HABARI ZAIDI KATIKA INTANETI www.watchtower.org

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 18 Ugonjwa wa ngozi ulioitwa ukoma nyakati za Biblia unatia ndani ule ambao leo unaitwa ugonjwa wa Hansen.