Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Epuka Marafiki Wabaya!

Epuka Marafiki Wabaya!

Kwa Ajili ya Vijana

Epuka Marafiki Wabaya!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Dina, Shekemu, Yakobo, Simeoni, na Lawi

Muhtasari: Dina ananajisiwa na Shekemu, na ndugu zake wenye hasira wanalipiza kisasi.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA MWANZO 34:1-31.

Unafikiri Dina alijihusisha na mambo gani akiwa na rafiki zake huko Kanaani?

․․․․․

Unafikiri ni maneno gani yenye ‘kushawishi’ ambayo Shekemu aliendelea kumwambia Dina?

․․․․․

Unatambua hisia gani wakati Yakobo anapowakemea Simeoni na Lawi katika mstari wa 30?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Unafikiri ni kwa nini Dina aliwatembelea mabinti wa Kanaani kwa ukawaida? (Kwa mfano, walishirikiana katika mambo gani? Alipata vitu gani miongoni mwa Wakanaani ambavyo hangeweza kupata kwao nyumbani?)

․․․․․

Ni sifa gani zenye kuvutia za Shekemu ambazo huenda Dina aliona? (Soma tena mstari wa 3, 12, na 19.)

․․․․․

Biblia inaonyeshaje kwamba Dina hakutaka kufanya ngono na Shekemu? (Soma tena mstari wa 2.)

․․․․․

Unafikiri ilikuwa sawa kwa Simeoni na Lawi kulipiza kisasi kwa kuwauwa wanaume wa jiji la Shekemu? Kwa nini?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Umuhimu wa kuchagua rafiki zako kwa busara.

․․․․․

Umuhimu wa kujizuia, hata kama una sababu nzuri ya kukasirika.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAYOWEZA KUTUMIA HABARI HIYO.

Unaweza kufanya nini ili kuepuka kutumiwa vibaya kingono na watu ambao hawathamini viwango vya Mungu vya maadili?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au soma habari zaidi katika Intaneti www.watchtower.org