Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hali Zitakuwa Nzuri Hivi Karibuni!

Hali Zitakuwa Nzuri Hivi Karibuni!

Hali Zitakuwa Nzuri Hivi Karibuni!

“Bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena . . . Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—ZABURI 37:10, 11.

JE, UNGEPENDA kuona unabii ambao umetajwa ukitimia? Bila shaka. Kuna sababu nzuri za kuamini kwamba utatimia hivi karibuni.

Makala zilizotangulia zilizungumzia baadhi ya unabii wa Biblia ambao unaonyesha waziwazi kwamba tunaishi katika “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5) Kupitia roho yake, Mungu aliwaongoza waandikaji wa Biblia watabiri matukio hayo ili tuwe na tumaini. (Waroma 15:4) Kutimia kwa unabii huo kunaonyesha kwamba matatizo tunayokabili sasa yataisha hivi karibuni.

Ni nini kitakachofuata baada ya siku za mwisho? Ufalme wa Mungu utatawala wanadamu wote. (Mathayo 6:9, 10) Ona maelezo ya Biblia kuhusu jinsi hali zitakavyokuwa duniani wakati huo:

Njaa itaisha. “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”—Zaburi 72:16.

Magonjwa yataondolewa. “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24.

Dunia itafanywa kuwa mpya. “Nyika na nchi isiyo na maji itafurahi; na nchi tambarare ya jangwani itakuwa na shangwe na kuchanua maua kama zafarani.”—Isaya 35:1.

Hayo ni mambo machache tu ya unabii mwingi wa Biblia ambao utatimia hivi karibuni. Tunakutia moyo uwaombe Mashahidi wa Yehova wakueleze sababu inayofanya wawe na hakika kwamba hali zitakuwa nzuri hivi karibuni.