Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yan Zabolotnyi/stock.adobe.com

ENDELEA KUKESHA!

Uhalifu Unaongezeka Ulimwenguni Pote—⁠Biblia Inasema Nini?

Uhalifu Unaongezeka Ulimwenguni Pote—⁠Biblia Inasema Nini?

 Magenge yanasababisha jeuri nchini Haiti. Uhalifu wenye jeuri umeenea nchini Afrika Kusini na Mexico, kutia ndani nchini nyingine za Amerika ya Latini. Hata katika maeneo ambako jeuri imepungua, ripoti kuhusu uhalifu dhidi ya mali zinawafanya watu wasijihisi salama na wawe na hofu.

 Biblia inasema nini kuhusu uhalifu unaotukia ulimwenguni pote?

Mambo ambayo Biblia ilitabiri kuhusu uhalifu

 Biblia ilitabiri kwamba uhalifu ungekuwa sehemu ya ishara ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3) Yesu alisema hivi alipofafanua matukio yaliyofanyiza ishara hiyo:

  •    “Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.”​—Mathayo 24:12, Biblia Habari Njema.

 Pia, Biblia ilitabiri kwamba “katika siku za mwisho” watu watakuwa “wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema.” (2 Timotheo 3:1-5) Tabia hizo za ubinafsi zinachangia uhalifu tunaoona leo.

 Lakini tuna sababu za kuwa na tumaini. Biblia inaahidi kwamba hivi karibuni hakutakuwa tena na uhalifu.

  •    “Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo. Lakini wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.”​—Zaburi 37:10, 11.

 Jifunze mengi zaidi kuhusu ujumbe wa Biblia wenye tumaini na kwa nini unaweza kuwa na uhakika kwamba matukio tunayoona leo yanatimiza unabii wa Biblia. Chunguza makala zifuatazo.

 Tumaini Bora la Wakati Ujao

 Ni Nini Ishara ya ‘Siku za Mwisho’?

 Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?