Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 1

Siri Ambayo Tunafurahi Kuijua

Siri Ambayo Tunafurahi Kuijua

Je, umewahi kuambiwa siri?— * Biblia inazungumza kuhusu siri ya pekee inayoitwa “siri takatifu.” Ni takatifu kwa sababu inatoka kwa Mungu. Na inaitwa siri kwa sababu watu hawakuijua. Hata malaika walitamani kujua mambo mengi kuhusu siri hiyo. Je, ungependa kuijua siri hiyo?—

Unafikiri malaika walikuwa wanataka kujua nini?

Hapo zamani za kale, Mungu alimuumba mwanaume na mwanamke wa kwanza. Waliitwa Adamu na Hawa. Mungu aliwapa mahali pazuri sana pa kuishi, mahali hapo paliitwa bustani ya Edeni. Kama Adamu na Hawa wangemtii Mungu, wao pamoja na watoto wao wangeifanya dunia nzima iwe paradiso. Na hivyo, wangeishi milele kwenye Paradiso. Lakini, je, unakumbuka Adamu na Hawa walifanya nini?—

Adamu na Hawa hawakumtii Mungu, hiyo ndiyo sababu leo hatuishi kwenye paradiso. Lakini Mungu alisema kwamba ataifanya dunia nzima iwe mahali pazuri sana, na kila mtu ataishi kwa furaha milele. Mungu atafanya hivyo jinsi gani? Kwa miaka mingi sana watu hawakujua jibu la swali hilo. Ilikuwa siri.

Yesu alipokuja duniani, aliwafundisha watu mambo mengi kuhusu siri hiyo. Alisema kwamba ilihusu Ufalme wa Mungu. Yesu aliwafundisha watu wasali Ufalme huo uje. Ufalme huo utaifanya dunia nzima iwe paradiso nzuri.

Je, umefurahi kuijua siri hiyo?— Kumbuka kwamba ni wale tu wanaomtii Yehova ndio watakaoishi katika Paradiso. Biblia inatuambia kuhusu wanaume na wanawake ambao walimtii Yehova. Je, ungependa kuwajua?— Sasa, ngoja tusome habari fulani kuhusu baadhi ya watu hao na jinsi tunavyoweza kuwaiga.

^ fu. 3 Baada ya kila maswali fulani katika masimulizi haya utaona alama hii (—). Huo ni wakati mzuri wa kutua kidogo na kumruhusu mtoto wako ajibu.