Ona video zinazopatikana

TAREHE 22 MWEZI 8, 2017
AUSTRIA

Muji Mumoja Katika Austria Unaonyesha Heshima Mashahidi wa Yehova 31, Wenye Waliteswa na Utawala wa Wanazi

Muji Mumoja Katika Austria Unaonyesha Heshima Mashahidi wa Yehova 31, Wenye Waliteswa na Utawala wa Wanazi

Meya wa muji wa Techelsberg, Johann Koban (katikati), anafunua jiwe la musingi la ukumbusho katika Techelsberg, pamoja na Peter Stocker (kuume) na gavana wa jimbo la Carinthia, Doktere Peter Kaiser (kushoto).

SELTERS, Ujerumani—Asubui, tarehe 19 Mwezi wa 5, 2017, katika muji wa Techelsberg, Austria, kulifanywa tukio la kukumbuka Mashahidi wa Yehova wenye Wanazi waliua ao kufunga katika kambi za mateso. Jiwe la musingi la ukumbusho lilionyeshwa wakati wa tukio hilo ili kuonyesha heshima kwa ajili ya Mashahidi 31 wa Techelsberg na maeneo ya karibu wenye walitendewa mubaya na Utawala wa Wanazi.”

Programu ilianzishwa na waimbaji 60 wenye waliimba wimbo wenye kichwa: “Songeni Mbele Enyi Mashahidi!” bila kutumia chombo fulani cha muziki. Mashahidi wa Yehova katika dunia yote wangali wanaimba leo wimbo huo katika ibada yao ya kila juma, wenye ulitungwa zamani katika kambi ya mateso katika Sachsenhausen na Erich Frost, Shahidi mwenye alifungwa na Wanazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Kisha muziki wa utangulizi, wageni mbalimbali wenye walialikwa, ni kusema, Johann Koban (meya wa muji Techelsberg), Peter Stocker (mujukuu ao munkana wa Gregor Wohlfahrt, mwenye alikuwa kati ya watu wa muji wa Techelsberg wenye walitendewa mubaya), Profesa Peter Gstettner, Profesa Vinzenz Jobst, na Doktere Peter Kaiser (gavana wa jimbo) walitoa hotuba mbele ya watu 350 hivi. Vyombo vya kutangaza habari vya Austria, ORF 2 na ORF Kärnten vilitangaza tukio hilo pamoja na magazeti mbalimbali ya kutangaza habari ya eneo hilo.

Profesa Peter Gstettner anatolea wahuzuriaji hotuba.

Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu Mashahidi 212 kati ya 550 katika Austria walipelekwa katika kambi za mateso kwa sababu walionwa kimakosa kuwa hatari kwa Utawala wa Ujerumani wa Wanazi kwa sababu ya musimamo wao wa kukataa kujiingiza katika mambo ya politike na kukataa kutegemeza vita. Katika kambi za mateso, Mashahidi wa Yehova walilazimishwa kuvaa kitambaa cha pembe tatu cha rangi ya zambarau (violet) kwenye nguo zao za wafungwa ili kuwatofautisha na wafungwa wengine. Mashahidi 154 wa Austria waliuawa katika maangamizi makubwa yenye yalifanywa na Wanazi.

Mbele tukio hilo lifanywe, majina ya Mashahidi tano wenye waliuawa na Wanazi (Johann Stossier, Anton Uran, Gregor Wohlfahrt, Gregor Wohlfahrt, na Willibald Wohlfahrt) yalikuwa kwenye ukumbusho fulani wa vita, kwenye liste ya “watu wenye walipotea,” jambo lenye haliko la kweli. Profesa Gstettner alieleza maana ya jiwe hilo la musingi kwa kusema hivi: “Hili linaonyesha ukweli wa historia na kutukumbusha wanaume hao wenye kupitia ujasiri wao mwingi na imani ya kweli walionyesha kama kukataa kabisa kuunga mukono utawala wenye kutendea watu mubaya kunakubaliwa kulingana na kanuni za mwenendo na kunafikia kuleta ushindi.”

Jiwe la musingi la ukumbusho kwa ajili ya Mashahidi wa Yehova 31 wenye waliuawa, kufungwa, ao wenye waliteswa na Wanazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Jiwe hilo liko na maneno yenye Franz Wohlfahrt aliandika (ona kisanduku hapa chini) na majina ya Mashahidi tano wa Techelsberg wenye majina yao yalikuwa zamani kwenye ukumbusho wa vita kwenye liste ya “watu wenye walipotea.”

Johann Zimmermann, musemaji wa Mashahidi wa Yehova katika Austria, anasema hivi: “Tunapendezwa na matukio kama haya yenye kuonyesha ujasiri na imani ya Mashahidi wa Yehova hata kama waliteswa mubaya sana. Tunatumaini kama tukio hili litasaidia watu wengi wakumbuke namna kikundi kidogo cha watu kinaweza kuteswa sana ikiwa kinaonwa kimakosa kuwa hatari kwa Serikali.”

Watangazaji wa habari wanaweza kuzungumuza na:

David A. Semonian, Biro ya Kutoa Habari, tel. +1-845-524-3000

Austria: Johann Zimmermann, tel. +43-1-804-53-45

Ujerumani: Wolfram Slupina, tel. +49-6483-41-3110