Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | BIBLIA INATOKA KABISA KWA MUNGU?

Biblia​—Inasema Kweli Katika Mambo Yote

Biblia​—Inasema Kweli Katika Mambo Yote

Inasema Kweli Katika Mambo ya Sayansi

HATA KAMA Biblia haiko kitabu cha sayansi, inasema kweli wakati inazungumuzia ulimwengu wa asili. Kwa mufano, tuzungumuzie hali ya hewa na chembe za uriti.

HALI YA HEWA​—NAMNA MVUA INATOKEA

HALI YA HEWA

Biblia inasema hivi: ‘[Mungu] anateka matone ya maji; yanajichuja kama mvua yakuwe ukungu wake; hivi kwamba mawingu yanadondoka [ao, yanaanguka chini].’​—Ayubu 36:27, 28.

Katika andiko hilo, Biblia inaonyesha hatua tatu za muzunguko wa maji. Mungu​—Chanzo cha joto ya jua​—‘anateka matone ya maji’ kupitia (1) uvukizaji (évaporation). Kisha, kupitia (2) kufanyizwa kwa matone, muvuke wa maji unapanda juu na kufanyiza mawingu, na mawingu hayo yanatokeza maji yenye yanaanguka kama mvua ao (3) yananyesha kwa njia ingine. Mupaka leo, wanasayansi wenye kujifunza hali ya hewa hawajaelewa kabisa mambo yote kuhusu namna mvua inatokea. Jambo la kufurahisha ni kwamba Biblia inauliza hivi: “Kwa kweli, ni nani anayeweza kuelewa tabaka za mawingu?” (Ayubu 36:29) Lakini, Muumbaji anaelewa kabisa muzunguko wa mvua na alihakikisha kama mwandikaji fulani aliandika mambo ya kweli kuhusu jambo hilo katika Biblia. Na alifanya hivyo zamani sana, mbele wanadamu wafikie kufasiria kisayansi hatua za musingi za kufanyizwa kwa mvua.

CHEMBE ZA URITI​—KUKOMAA KWA KIINI-TETE CHA MWANADAMU

CHEMBE ZA URITI

Mufalme Daudi, mumoja kati ya waandikaji wa Biblia, alimuambia Mungu hivi: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa.” (Zaburi 139:16) Katika zaburi hiyo, Daudi anaonyesha kwamba kiini-tete kinakomaa kwa kufuata maagizo fulani yenye yaliandikwa katika “kitabu,” ao plan. Jambo la kushangaza ni kwamba, maneno hayo yaliandikwa kumepita miaka 3 000 hivi!

Lakini, ni katika mwaka wa 1860 hivi tu ndio Gregor Mendel, mwanasayansi wa inchi ya Autriche, alivumbua kanuni za musingi za chembe za uriti. Na ni katika Mwezi wa Ine, mwaka wa 2003 tu, ndio wanasayansi walimaliza kufanya uchunguzi juu ya muundo wa génome ya mwanadamu, yenye kuwa na habari zote za lazima kuhusu chembe za uriti ili kufanyiza mwili wa mwanadamu. Wanasayansi wamelinganisha kemikali yenye kuwa na habari kuhusu chembe za uriti na kamusi yenye kujaa maneno ambayo yanafanyizwa na herufi za alfabeti. Maneno hayo yanafanyiza maagizo ya chembe za uriti. Kwa kufuata maagizo hayo, sehemu za kiini-tete, kama vile ubongo, moyo, mapafu, miguu na mikono, zinakomaa kwa utaratibu kabisa na kwa wakati wenye kufaa. Ni jambo lenye kufaa kwamba, wanasayansi fulani wamesema kama chembe za uriti ni kama “kitabu cha uzima.” Sababu gani muandikaji wa Biblia, Daudi, alifikia kusema maneno hayo bila kukosea? Kwa unyenyekevu alisema hivi: “Roho ya Yehova ndiyo iliyosema kupitia mimi, na neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.” *​— 2 Samweli 23:2.

Inatabiri Bila Kukosea Kuhusu Wakati Wenye Kuja

NI VIGUMU sana, ao hata haiwezekane, kujua wakati gani, namna gani, na kadiri gani falme na miji itatokea ao kuanguka. Lakini, Biblia ilitabiri kwa njia yenye kuwa wazi kuhusu kuharibiwa kwa falme na miji yenye nguvu. Tuchunguze mifano mbili tu.

KUANGUKA NA KUBAKI BILA KUKALIWA KWA MUJI WA BABILONI

Babiloni ya zamani ilikuwa muji mukubwa wa utawala wenye nguvu ambao ulitawala mangaribi ya Asia kwa miaka mingi. Wakati fulani, muji wa Babiloni ndio ulikuwa muji mukubwa kuliko miji yote katika dunia. Lakini, miaka 200 hivi mbele, Mungu aliongoza Isaya, muandikaji mumoja wa Biblia, atabiri kwamba mupiganaji mwenye kuitwa Koreshi angeharibu muji wa Babiloni na kwamba muji huo ungefikia kubaki bila kukaliwa milele. (Isaya 13:17-20; 44:27, 28; 45:1, 2) Jambo hilo lilitokea kabisa?

HISTORIA

Usiku moja, katika Mwezi wa 10, mwaka wa 539 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Koreshi Mukubwa alikamata muji wa Babiloni. Kadiri wakati ulipita, mifereji yenye ilikuwa inapeleka maji katika eneo la mbolea lenye kuzunguka Babiloni haikuhangaikiwa tena, na mifereji hiyo ikafikia kufungana. Inasemekana kwamba eneo hilo lilikuwa halikaliwe tena katika mwaka wa 200 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Leo, Babiloni ni mabomoko tu. Kama vile tu Biblia ilitabiri, Babiloni ‘imekuwa mahame yenye ukiwa.’​—Yeremia 50:13.

Namna gani muandikaji huyo wa Biblia alijua mbele ya wakati mambo hayo ya kweli kihistoria? Biblia inaonyesha kwamba hilo lilikuwa “tangazo juu ya Babiloni ambalo Isaya mwana wa Amozi aliona katika maono.”​—Isaya 13:1.

NINAWI​—“ENEO LISILO NA MAJI KAMA NYIKA”

Ninawi, muji mukuu wa Utawala wa Ashuru, ulionwa kuwa muji wenye kujengwa kwa njia ya ajabu. Muji huo ulikuwa na barabara kubwa-kubwa, bustani kwa ajili ya watu wote, mahekalu, na majengo makubwa-makubwa ya kifalme. Lakini, nabii Sefania alitabiri kwamba muji huo wenye kupendeza ungekuwa “mahame yenye ukiwa, eneo lisilo na maji kama nyika.”​—Sefania 2:13-15.

Majeshi ya Wababiloni na Wamedi yaliungana ili kuharibu muji wa Ninawi katika kipindi kati ya mwaka wa 700 na 601 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Kulingana na kitabu kimoja, muji huo wenye ulishindwa “ulisahauliwa kwa muda wa miaka 2 500.” Kwa muda fulani, watu walikuwa na mashaka kama muji wa Ninawi ulikuwaka kabisa! Ni katika mwaka wa 1850 hivi tu ndio wachimbuaji walichimbua mabomoko ya Ninawi. Leo, eneo hilo linaendelea kuharibika, hivi kwamba shirika la Global Heritage Fund limesema hivi: “Vitu vya zamani vyenye kubakia katika Ninawi vinaweza kuzikwa tena milele.”

Namna gani Sefania alijua jambo hilo mbele ya wakati? Alikubali kwamba ilikuwa ‘neno la Yehova lililomujia.’​—Sefania 1:1.

Biblia Inajibia Maulizo ya Maana Sana Kuhusu Maisha

BIBLIA inajibia kwa njia yenye kufurahisha maulizo ya maana sana kuhusu maisha. Tuchunguze mifano yenye kufuata.

SABABU GANI KUNA UBAYA NA MATESO MENGI KATIKA DUNIA?

Habari kuhusu ubaya na mateso inazungumuziwa sana katika Maandiko. Biblia inaonyesha kwamba:

  1. ‘Mwanadamu amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’​Mhubiri 8:9.

    Utawala mubaya wa mwanadamu umeleta mateso mengi sana.

  2. “Wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.”​Mhubiri 9:11.

    Matukio yenye hayatazamiwe​—kama vile magonjwa, aksidenti, ao misiba​—yanaweza kupata mutu yeyote, kutokea nafasi yoyote, na kwa wakati wowote.

  3. ‘Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi.’ ​Waroma 5:12.

    Wakati mwanaume na mwanamuke wa kwanza waliumbwa, hakukuwa zambi na kifo. Zambi “iliingia katika ulimwengu” wakati walikataa kutii kimakusudi Muumbaji wao.

Biblia haifasirie tu sababu gani tunateseka. Inaahidi pia kwamba Mungu atamaliza mateso na “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:3, 4.

NI NINI INATOKEA WAKATI MUTU ANAKUFA?

Biblia inaonyesha kwamba kifo ni hali ya kutojua jambo lolote na kutokuwa na utendaji wowote. Andiko la Mhubiri 9:5 linasema hivi: “Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe.” Wakati mutu anakufa, ‘mawazo yake yanapotea.’ (Zaburi 146:4) Kwa hiyo, wakati mutu anakufa, ubongo wake unaacha kufanya kazi yake yote, kutia ndani uwezo wake wa kuona, kusikia, kuonja, kugusa, na kunusa. Ndiyo sababu wakati mutu anakufa hawezi tena kufanya jambo lolote, kuwa na hisia, ao kuwaza.

Lakini, Biblia haifasirie tu hali ya wafu. Inaonyesha pia kwamba kuna tumaini nzuri la watu kuamuka kutoka katika usingizi wa kifo kupitia ufufuo.​—Hosea 13:14; Yohana 11:11-14.

MAISHA YANA KUSUDI GANI?

Kulingana na Biblia, Yehova Mungu aliumba mwanaume na mwanamuke. (Mwanzo 1:27) Adamu, mwanaume wa kwanza, anaitwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Mwanadamu aliumbwa kwa kusudi hili: Kuwa na urafiki pamoja na Baba yake wa mbinguni na kuishi milele duniani akiwa na maisha mazuri na yenye furaha. Ndiyo sababu wanadamu wote waliumbwa na uwezo wa kiroho, ni kusema, tamaa ya kutaka kujua Mungu. Kwa hiyo, Biblia inasema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”​—Mathayo 5:3.

Zaidi ya hilo, Biblia inasema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!” (Luka 11:28) Biblia haitufundishe tu kuhusu Mungu, lakini inatusaidia pia kuishi maisha yenye furaha na inatupatia tumaini kuhusu wakati wenye kuja.

Mutungaji wa Biblia na Wewe

KISHA kuchunguza ushuhuda mbalimbali, mamilioni ya watu katika dunia wamefikia kuwa hakika kwamba Biblia haiko tu kitabu cha zamani. Wako hakika kwamba Biblia ni Neno la Mungu lenye kuongozwa na roho, ni kusema, njia yake ya kuzungumuza na wanadamu wote, kutia ndani na wewe! Katika Biblia Mungu anakualika ufikie kumujua na ukuwe rafiki yake. Biblia inaahidi hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’​—Yakobo 4:8.

Kujifunza Biblia kwa uangalifu kutakusaidia sana. Namna gani? Kama vile tu kusoma kitabu fulani kunaweza kukusaidia ujue kwa kiasi fulani mawazo ya muandikaji wa kitabu hicho, kusoma Biblia kunafunua mawazo ya Mungu, Mutungaji wa Biblia, na namna anajisikia. Fikiria faida yenye unaweza kupata. Unaweza kufikia kujua mawazo ya Muumbaji wako na namna anajisikia! Tena, Biblia inafunua:

Utapenda kujua mambo mengi zaidi? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia. Watakamata mipango ili ujifunze Biblia bila kulipa. Hilo litakusaidia umukaribie zaidi Yehova Mungu, Mutungaji wa Biblia.

Habari hii ilionyesha ushuhuda fulani wenye kuhakikisha kwamba Biblia ni kitabu chenye kuongozwa na roho. Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 2 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na kinapatikana pia kwenye www.ps8318.com

Unaweza pia kuangalia video Ni Nani Aliandikisha Biblia? yenye kupatikana kwenye www.ps8318.com

Fungua kichwa VICHAPO > VIDEO

^ fu. 10 Katika Biblia, Mungu anajulikana kwa jina lake la pekee, Yehova.​—Zaburi 83:18.