Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAONI YA BIBLIA

Shetani

Shetani

Je, Shetani ni mutu anayeishi kwelikweli?

“Yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.”​—Ufunuo 12:9.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA

Watu fulani wanaamini kwamba Shetani si mutu, lakini ni ubaya ulio ndani ya kila mutu.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Shetani ni mutu anayeishi kwelikweli. Ni malaika muasi, kiumbe wa kiroho anayemupinga Mungu. Biblia inamuita Shetani ‘mutawala wa ulimwengu huu.’ (Yohana 12:31) Anatumia ‘ishara za uongo’ na “udanganyifu” ili kutimiza makusudi yake.​—2 Wathesalonike 2:9, 10.

Biblia inasema juu ya mazungumuzo yaliyokuwa kati ya Shetani na Mungu huko mbinguni. Ikiwa Shetani angekuwa tu ubaya ulio ndani ya kila mutu, namna gani Mungu, ambaye ni mukamilifu na mutakatifu, angeweza kuzungumuza na ubaya fulani ulio ndani yake? (Kumbukumbu la Torati 32:4; Ayubu 2:1-6) Ni wazi kwamba Shetani ni mutu anayeishi kwelikweli, yeye si ubaya ulio ndani ya watu.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Shetani anataka uamini kwamba yeye si mutu anayeishi kwelikweli; ni kama vile mutu mubaya anayeficha yeye ni nani ili aendelee kuvunja sheria bila kuvumbuliwa. Ili kujilinda na Shetani, ni lazima utambue kwanza kwamba yeye ni mutu anayeishi kwelikweli.

Shetani anaishi wapi?

“Ole wa dunia . . . kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu.”​—Ufunuo 12:12.

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA

Watu wengi wanaamini kwamba Shetani anaishi katika moto wa mateso chini ya udongo. Wengine wanawaza kwamba anakaa ndani ya watu wabaya.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Shetani ni kiumbe wa roho, kwa hiyo anaishi mahali pasipoonekana. Kwa wakati fulani, Shetani aliruhusiwa kufika mbinguni mahali ambapo Mungu na malaika waaminifu wanaishi, wakati wowote alipotaka. (Ayubu 1:6) Lakini sasa haruhusiwe tena kufika mbele za Mungu na ametupwa chini katika ujirani wa dunia pamoja na mashetani wengine.​—Ufunuo 12:12.

Je, ni kusema kama Shetani anaishi mahali fulani duniani? Kwa mufano, labda umekwisha kusoma kwamba Biblia inautaja muji wa zamani wa Pergamamu “mahali anapokaa Shetani.” (Ufunuo 2:13) Lakini kwa kweli, maneno hayo yanaonyesha tu kwamba katika muji huo ibada ya Shetani ilienea sana. Shetani haishi mahali fulani duniani. Biblia inasema kwamba “falme zote za dunia inayokaliwa” ni zake.​—Luka 4:5, 6.

Je, Shetani anaweza kuwatendea watu vibaya ao kuwatawala?

‘Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’​—1 Yohana 5:19.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Watu wengi wamejiacha waongozwe na Shetani na kwa hiyo wametawaliwa naye. (2 Wakorintho 11:14) Jambo hilo linatusaidia kuelewa sababu gani wanadamu wameshindwa kutengeneza hali za dunia.

Biblia inazungumuzia pia watu walioingiwa na Shetani ao malaika wengine waasi, na mashetani hao waliwafanya wateseke.​—Mathayo 12:22; 17:15-18; Marko 5:2-5.

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Hauna sababu ya kuogopa nguvu za Shetani. Ili Shetani asikutawale, ni lazima ujifunze njia anazotumia ili kuwadanganya watu, kwa hiyo ‘hautakosa kuzijua mbinu zake.’ (2 Wakorintho 2:11) Kwa kusoma Biblia, unaweza kujua njia ambazo Shetani anatumia ili kuwadanganya watu na hivyo kuziepuka.

Jiepushe na kila kitu kinachohusiana na kazi za mashetani. (Matendo 19:19) Vitu hivyo vinaweza kuwa hirizi, vitabu, video, miziki, na programu za ordinatere zilizo na mambo ya uchawi ao uaguzi.

Biblia inasema, ‘mupingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.’ (Yakobo 4:7) Kwa kutii shauri hilo lenye hekima la Biblia, unaweza kujilinda na hila za Shetani.​—Waefeso 6:11-18.

[Caption on page 6]

Tafuta majibu mengine ya maulizo juu ya habari za Biblia kwenye adresi yetu ya Internete www.ps8318.com