Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Wanyama

Wanyama

Kwa njia fulani, wanyama wanatimiza jambo fulani katika maisha ya kila mutu. Tunaweza kutendea wanyama namna tunapenda?

Watu wanapaswa kutendea wanyama namna gani?

MAMBO WATU WANASEMA

Watu fulani wanasema kama wanadamu wanaweza kutumikisha wanyama kwa njia yenye wanaona inafaa. Wengine wanaona kuwa wanyama wanapaswa kutendewa kama vile tu wanadamu.

  • Mutu mumoja mwenye kujulikana sana anayetetea haki za wanyama alisema kama wanyama wanapaswa “kupewa haki ya musingi, hawapaswe kutendewa tu kama mali ao biashara ya kuleta feza.” Alisema tena hivi: “Hatupaswe kutendea wanyama kama vile ni vitu vyetu.”

  • Leona Helmsley ambaye alikuwa na utajiri wa mamiliare ya dola, alifanya jambo fulani lenye watu wengi waliona kuwa lilipitisha mipaka. Aliachia imbwa yake uriti wa dola milioni 12 na aliomba maiti ya imbwa hiyo izikwe karibu na maiti yake wakati itakufa.

Jambo la kufikiria: Unawaza wanyama wanapaswa kutendewa namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Yehova Mungu, Muumbaji wa uzima, aliambia wanadamu “Watawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.” (Mwanzo 1:28) Kwa hiyo, ni jambo lenye kupatana na akili kusema kama Mungu anaona kuwa wanadamu ni wa maana kupita wanyama.

Andiko lenye linatangulia andiko lenye tumekwisha kutaja, linahakikisha hata zaidi jambo hilo. Biblia inasema kuwa ‘Mungu alimuumba mutu kwa mufano wake, kwa mufano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.’—Mwanzo 1:27.

Kwa kuwa tuliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu,’ sisi tu ndio tunaweza kuonyesha sifa za Mungu kama vile, hekima, haki, na upendo. Pia, tunazaliwa na uwezo wa kuchagua mwenendo muzuri na kuabudu Mungu. Wanyama hawana uwezo kama huo kwa sababu hawakuumbwa ‘kwa mufano wa Mungu.’ Wanyama ni wa hali ya chini kwa kuwalinganisha na wanadamu na hawapaswe kutendewa sawasawa na wanadamu.

Hilo linamaanisha kuwa wanadamu wako na haki ya kutesa wanyama? Hapana.

‘Siku sita utafanya kazi yako; lakini siku ya saba utaacha, ili ngombe-dume wako na punda wako wapate kupumuzika’Kutoka 23:12.

Ni mubaya kuua wanyama?

MAMBO WATU WANASEMA

Watu fulani wenye kuwinda wanyama ao kulowa samaki wanaua wanyama ili kufanya michezo, kujifurahisha ao kufanya mashindano. Watu wengine wanakubaliana na mawazo haya ya Leo Tolstoy, muandikaji wa vitabu wa Urusi, ambaye aliandika kama kuua na kukula wanyama ni “mwenendo mubaya.”

MAMBO BIBLIA INASEMA

Mungu anaruhusu watu waue wanyama ili kulinda uzima wa wanadamu ao ili kupata vitu vya kutengeneza manguo. (Kutoka 21:28; Marko 1:6) Pia Biblia inasema kama watu wanaweza kuua wanyama kwa ajili ya chakula. Andiko la Mwanzo 9:3 linasema hivi: ‘Kila munyama anayetembea ambaye yuko hai anaweza kuwa chakula chenu.’ Hata Yesu alisaidia wafuasi wake kulowa samaki ambazo walikula baadaye.—Yohana 21:4-13.

Lakini Biblia inasema kama Mungu anachukia ‘mutu yeyote anayependa jeuri.’ (Zaburi 11:5) Kwa hiyo tunaweza kusema kama Mungu hapendi tuumize ao kuua wanyama ili tu kujifurahisha ao kwa ajili ya michezo.

Biblia inaonyesha kama Mungu anaona uzima wa wanyama kuwa wa maana sana.

  • Biblia inasema kama wakati wa uumbaji, ‘Mungu alifanya munyama-mwitu wa dunia kulingana na aina yake na munyama wa kufugwa kulingana na aina yake na kila munyama anayetembea wa inchi kulingana na aina yake. Mungu akaona ya kuwa ilikuwa vyema.’Mwanzo 1:25.

  • Biblia inasema kama Yehova “anawapa wanyama chakula.” (Zaburi 147:9) Mungu aliumba dunia kwa njia ambayo inaweza kutoa chakula na makao ya kutosha kwa ajili ya wanyama.

  • Mufalme Daudi wa Israeli alisema hivi katika sala: ‘Wewe unaokoa mwanadamu na munyama, Ee Yehova.’ (Zaburi 36:6) Kwa mufano, wakati wa Garika ya duniani pote, Yehova alilinda watu munane na kila aina ya wanyama mbele aharibu watu wabaya.—Mwanzo 6:19.

Bila shaka, Yehova ambaye aliumba wanyama anapendezwa nao, na anatazamia wanadamu watendee wanyama kwa heshima yenye kuwastahili.

‘Mwadilifu anatunza nafsi ya munyama wake wa kufugwa.’Methali 12:10.