Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Habari Fulani Juu ya Mazingira

Habari Fulani Juu ya Mazingira

Hata kama dunia inatoa hewa ya muzuri, chakula kizuri, na maji safi, wanadamu wanaendelea kuvuruga mambo hayo ya asili. Wanasayansi wanaendelea kutafuta sana namna ya kulinda mazingira.

AUSTRALIA

Inakadiriwa kuwa maji mengi (500000 km3) yasiyokuwa na chumvi nyingi yanapatikana chini ya udongo wa bahari za dunia. Vincent Post wa Masomo ya Juu ya Flinders katika muji wa Adelaide anasema kama “maji ya bahari yalikuwa chini sana kuliko leo,” kwa hiyo sehemu ya pembeni ya bahari ilikuwa mbali. Wakati huo, mvua ilikuwa “inajaza sehemu za maji zenye kuwa chini ya udongo katika maeneo ambayo leo yanapatikana chini ya bahari.” Wanasayansi wanaamini kuwa maji hayo yenye kuwa chini ya udongo wa bahari wakati fulani yanaweza kusaidia watu zaidi ya milioni 700 wenye kuwa na magumu ya kupata maji safi.

JANGWA LA SAHARA

Karibu nusu ya aina za wanyama wakubwa-wakubwa wenye walikuwa katika jangwa la Sahara wameisha, ao sasa wamepoteza sehemu 99 juu ya 100 (99%) ya makao yao. Kukosa usalama katika eneo hilo na kuwinda sana wanyama ni kati ya sababu zenye kutokeza jambo hilo. Hata ikiwa wanyama na mimea yenye kuwa katika jangwa ni sawa na ile yenye kuwa katika pori, wachunguzi wanasema kama “wanasayansi hawahangaikie sana jangwa kwa sababu ya kukosa musaada wa feza.” Hilo linafanya ikuwe vigumu kwa watu wenye kuchunga mazingira kulinda mimea ao wanyama wa jangwa wenye kuwa katika hatari.

ULIMWENGU

Imekadiriwa kuwa mutu 1 kati ya kila watu 8 wenye walikufa katika mwaka wa 2012, alikufa kwa sababu ya kuchafuliwa kwa hewa. Shirika la Afya Ulimwenguni (OMS) linaonyesha kuwa “leo, kuchafuliwa kwa hewa ndilo tatizo kubwa zaidi katika mazingira lenye linatia afya katika hatari.”