Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Usijiingize Katika Mambo ya Politike ya Ulimwengu huu Wenye Kugawanyika

Usijiingize Katika Mambo ya Politike ya Ulimwengu huu Wenye Kugawanyika

Mumulipe . . . Mungu vitu vya Mungu.MATHAYO 22:21.

NYIMBO: 33, 137

1. Namna gani tunaweza kutii Mungu na serikali za wanadamu?

BIBLIA inatufundisha kutii serikali ao guvernema za wanadamu, lakini inatuambia pia kama tunapaswa kumutii Mungu sikuzote. (Matendo 5:29; Tito 3:1) Tunaweza kufanya hivyo namna gani? Yesu alieleza kanuni yenye inatusaidia kujua ni nani mwenye tunapaswa kutii. Alisema kama tunapaswa kumulipa “Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.” [1] (Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.) (Mathayo 22:Tunamulipa “Kaisari vitu vya Kaisari” wakati tunatii sheria za serikali, wakati tunaheshimu wakubwa wa serikali, na wakati tunalipa kodi (taxe). (Waroma 13:7) Lakini wakati serikali inatuomba tufanye jambo fulani lenye Mungu hapendi tufanye, tunakataa kufanya jambo hilo, lakini sikuzote tunakataa kwa heshima.

2 Njia moja yenye tunamulipa “Mungu vitu vya Mungu” ni kukataa kuunga mukono mambo ya politike ya ulimwengu huu. Hatujiingize katika mambo hayo. (Isaya 2:4) Kwa sababu Yehova anaacha serikali za wanadamu zitawale, tunapaswa kuzitii. Pia, hatujiingize katika mambo yote yenye kuonyesha kama tunapenda sana inchi yetu ao taifa letu. (Waroma 13:1,2) Hatujaribu kubadilisha serikali ao kuchochea wakubwa wa politike, na hatuchague mutu yeyote wa chama fulani cha politike ao kufanya politike.

3. Sababu gani hatupaswe kujiingiza katika mambo ya politike?

3 Kuko sababu nyingi zenye kufanya Mungu atukataze kujiingiza katika mambo ya politike. Sababu moja ni hii: tunamuiga Yesu, yeye hakukuwa “sehemu ya ulimwengu.” Hakuunga mukono hata kidogo mambo ya politike ao mambo ya vita. (Yohana 6:15; 17:16) Sababu ingine ni hii: tunaunga mukono Ufalme wa Mungu. Kwa sababu hatuunge mukono serikali za wanadamu, tuko na zamiri safi wakati tunahubiria watu kama ni Ufalme wa Mungu tu ndio utamaliza magumu yote ya wanadamu. Dini za uongo zinajiingiza katika mambo ya politike ya ulimwengu huu, na hilo linaletea watu migawanyiko. Lakini kwa sababu hatujiingize katika mambo ya politike, tunaishi katika umoja na ndugu na dada zetu katika dunia yote.—1 Petro 2:17.

4. (a)Namna gani tunajua kama tutapambana sana na jaribu la kutukaza tujiingize katika mambo ya politike? (b)Sababu gani tunapaswa kujitayarisha leo ili tuepuke kujiingiza katika mambo ya politike?

4 Pengine tunaishi mahali penye watu hawatulazimishe tujiingize katika mambo ya politike. Lakini, kwa sababu tunaendelea kukaribia mwisho wa ulimwengu wa Shetani, itakuwa vigumu zaidi kwetu kukataa kujiingiza katika mambo ya politike. Leo, watu ‘hawataki makubaliano’ na ni “wenye vichwa vigumu,” na wataendelea kuwa na migawanyiko sana. (2 Timotheo 3:3, 4) Katika inchi fulani kumetokea mabadiliko ya kushitukia katika mambo ya politike, na ndugu na dada wamepata magumu kwa sababu ya kukataa kujiingiza katika mambo ya politike. Ndiyo sababu tunapaswa kujitayarisha leo ili kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike hata wakati wa magumu. Tuzungumuzie basi mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kujitayarisha.

UONE SERIKALI ZA WANADAMU NAMNA YEHOVA ANAZIONA

5. Yehova anaona namna gani serikali za wanadamu?

5 Njia moja ya kujitayarisha leo ili kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike, ni kuona serikali za wanadamu namna Yehova anaziona. Wakati Yehova aliumba wanadamu, hakuwapatia haki ya kutawala wengine. (Yeremia 10:23) Anaona wanadamu wote kuwa familia moja. Lakini serikali za wanadamu zimeleta migawanyiko kati ya watu kwa sababu zinaonyesha kama taifa fulani ni la muzuri zaidi kuliko taifa lingine. Serikali fulani zinaonekana kuwa ni za muzuri, lakini haziwezi kumaliza magumu yote ya wanadamu. Pia, serikali za wanadamu zimepinga Ufalme wa Mungu wenye ulianza kutawala katika mwaka 1914. Hivi karibuni, Ufalme huo utaondoa serikali hizo zote za wanadamu.—Soma Zaburi 2:2, 7-9.

Ujitayarishe leo ili kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike hata wakati wa magumu

6. Namna gani tunapaswa kuona wale wenye kuwa na mamlaka katika serikali za wanadamu?

6 Mungu anaacha serikali za wanadamu zitawale kwa sababu zinasaidia kuleta utaratibu na amani kwa kiasi fulani. Jambo hilo linatusaidia tuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Waroma 13:3, 4) Mungu anatuambia hata tusali kwa ajili ya wale wenye kuwa na mamlaka ili tumuabudu katika amani. (1 Timotheo 2:1, 2) Wakati tunatendewa bila haki, tunaweza kuomba wenye kuwa na mamlaka katika serikali watusaidie. Mutume Paulo alifanya vile. (Matendo 25:11) Biblia inasema kama Shetani ndiye anaongoza serikali za wanadamu, lakini haiseme hata kidogo kama anaongoza kila mutu mwenye kuwa na mamlaka katika serikali hizo. (Luka 4:5, 6) Kwa hiyo, hatuwezi kuambia mutu yeyote kama mukubwa fulani wa serikali anaongozwa na Shetani. Biblia inatukataza kutukana ao kusema mubaya juu ya wengine.—Tito 3:1, 2.

7. Ni mawazo gani tunapaswa kuepuka?

7 Tunatii Mungu wakati tunakataa kuunga mukono mukubwa fulani wa politike, ao chama fulani cha politike, hata kama mawazo yao yanaweza kutuletea faida. Wakati fulani, inaweza kuwa vigumu kufanya vile. Kwa mufano, wazia kuwa watu wanapinga serikali fulani yenye imetesa watu sana, na hata Mashahidi wa Yehova. Kwa kweli, hautaunga mukono waasi hao, lakini, utafikiri kama wako na haki ya kufanya hivyo na kutumaini kama watapata matokeo ya muzuri? (Waefeso 2:2) Ikiwa hatupendi kabisa kujiingiza katika mambo ya politike, tunapaswa kuepuka kufikiri kama upande fulani ni wa muzuri zaidi kuliko upande mwingine. Tutaonyesha hivyo kupitia maneno na matendo yetu.

MUKUWE ‘WENYE KUJIHAZARI’ LAKINI “WASIO NA HATIA”

8 Njia ya pili yenye tunaepuka kujiingiza katika mambo ya politike ya ulimwengu ni kuwa ‘wenye kujihazari [waangalifu] kama nyoka na hata hivyo wasio na hatia [wasio na kosa] kama njiwa.’ (Soma Mathayo 10:16, 17.) Tuko ‘wenye kujihazari’ wakati tunafikiria mbele ya wakati hali zenye hatari. Na tuko “wasio na hatia” wakati hatuache hali hizo zituingize katika mambo ya politike. Tuzungumuzie basi hali fulani zenye hatari na mambo yenye tunaweza kufanya ili tusijiingize kabisa katika mambo ya politike.

9. Wakati tunazungumuza na wengine, tunapaswa kuwa waangalifu juu ya mambo gani?

9 Mazungumuzo. Tunapaswa kuwa waangalifu sana wakati watu wanaanza kuzungumuzia mambo ya politike. Kwa mufano, wakati tunazungumuza na mutu fulani juu ya Ufalme wa Mungu, tutaepuka kusema kama tunakubaliana ao tunakataa mawazo ya mukubwa fulani wa politike ao ya chama fulani cha politike. Kuliko kuzungumuzia mambo yenye wanadamu wanapenda kufanya ili kumaliza magumu ya wanadamu wenzao, tunatumia Biblia ili kuonyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya ili kumaliza kabisa magumu hayo. Ikiwa watu wanabishana juu ya mambo kama vile, ndoa ya mwanaume na mwanaume ao mwanamuke na mwanamuke, ao kutosha mimba, tunawaambia mambo yenye Neno la Mungu linasema na namna tunajikaza kutumikisha mambo hayo katika maisha yetu. Wakati mutu fulani anasema kama sheria fulani zinapaswa kuondoshwa ao kubadilishwa, hatumuunge mukono, na hatumukaze abadilishe mawazo yake.

Linganisha mambo yenye unasikia na “maneno yenye afya” yenye kupatikana katika Biblia

10. Namna gani tunaweza kuhakikisha kama hatuunge mukono mambo ya politike wakati tunasoma ao kufuata habari fulani?

10 Vyombo vya kutangaza habari. Wakati fulani, habari inatolewa katika njia yenye kuunga kabisa mukono upande fulani. Jambo hilo linafanyika zaidi sana katika inchi kwenye serikali inaongoza vyombo vya kutangaza habari. Ikiwa shirika fulani ao watangazaji wa habari wanaunga mukono upande fulani, tunapaswa kuwa waangalifu tusianze kufikiri kama wao. Kwa mufano, ujiulize hivi, ‘Ninafurahia kusikiliza mutangazaji wa habari fulani kwa sababu ninakubaliana na mambo yenye anasema juu ya politike?’ Ili kukusaidia usijiingize katika mambo ya politike, epuka kufuata ao kusoma habari zenye kuunga mukono upande fulani katika mambo ya politike. Lakini, ujikaze kutafuta habari zenye haziunge mukono upande fulani. Na sikuzote linganisha mambo yenye unasikia na “maneno yenye afya” yenye kupatikana katika Biblia.—2 Timotheo 1:13.

11.Namna gani inaweza vigumu kwetu kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike wakati tunaona vitu vyenye tuko navyo ni vya maana sana?

11 Kupenda vitu vya kimwili. Wakati tunaona kama feza na vitu vyenye tuko navyo ni vya maana sana, inaweza kuwa vigumu kwetu kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike. Kisha mwaka wa 1970, Mashahidi wengi wa Yehova katika inchi ya Malawi walipaswa kuacha vitu vyao vyote kwa sababu walikataa kuunga mukono chama fulani cha politike. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba wamoja kati yao hawakupenda kuacha maisha yao ya muzuri. Dada mumoja mwenye kuitwa Ruth anakumbuka hivi: “Wamoja walienda katika inchi ingine pamoja na sisi lakini kisha waliunga mukono chama fulani cha politike, na wakarudia kwao kwa sababu hawakupenda kuvumilia maisha magumu katika kambi.” Lakini watumishi wengi wa Mungu hawafanye hivyo. Hawajiingize katika mambo ya politike, hata kama hilo linafanya wakose feza ao kupoteza vitu vyao.—Waebrania 10:34.

12, 13. (a)Namna gani Yehova anaona wanadamu? (b) Namna gani tunaweza kujua ikiwa tumeanza kujivunia sana inchi yetu?

12 Majivuno. Kwa kawaida watu wanajivunia rangi yao ya ngozi, kabila, desturi, muji, ao inchi yao. Lakini Yehova haone kikundi fulani ao mutu fulani kuwa wa muzuri zaidi kuliko mwengine. Anaona watu wote kuwa sawasawa. Kwa kweli, Yehova aliumba kila mutu tofauti na mwengine, na tunaweza kufurahia tofauti hizo. Yehova hatuombe tuache desturi zetu. Lakini hapendi pia tufikiri kuwa sisi ni wazuri zaidi kuliko wengine.—Waroma 10:12.

13 Hatupaswe hata kidogo kujivunia sana inchi ao taifa letu na kufikiri kama inchi ao taifa letu ndilo la muzuri zaidi. Ikiwa tunafikiri vile, inaweza kuwa vigumu kwetu kuepuka kuunga mukono upande fulani. Jambo hilo lilitokea katika siku za mitume. Ndugu fulani Waebrania hawakuwatendea muzuri dada Wagiriki wenye walikuwa wajane. (Matendo 6:1) Namna gani tunaweza kujua ikiwa tumeanza kuwa na majivuno kama hayo? Ikiwa ndugu ao dada kutoka katika eneo lingine anakupatia mashauri fulani, utasema mara moja kwamba, ‘Sisi tunafanya muzuri sana mambo yote hapa’ na kisha unakataa mashauri hayo? Ikiwa ni hivyo, usisahau shauri hili la maana: ‘Kwa unyenyekevu wa akili muwaone wengine kuwa ni bora [maana zaidi] kuliko ninyi.’—Wafilipi 2:3.

YEHOVA ATAKUSAIDIA

14. Namna gani sala inaweza kutusaidia, na ni mufano gani wa Biblia wenye kuonyesha jambo hilo?

14 Njia ya tatu yenye tunaepuka kujiingiza katika mambo ya politike ni kumutegemea Yehova. Umuombe akupatie roho takatifu, kwa sababu roho hiyo inaweza kukusaidia ukuwe na sifa ya uvumilivu na kujizuia. Sifa hizo zitakusaidia wakati serikali inakutendea mubaya ao bila haki. Umuombe Yehova akupatie hekima ili utambue hali yenye inaweza kufanya ikuwe vigumu kwako kuepuka kujiingiza katika mambo ya politike. Tena umuombe akusaidie ufanye mambo mema katika hali hizo. (Yakobo 1:5) Unaweza kufungwa katika gereza ao kupewa malipizi fulani kwa sababu unabakia muaminifu kwa Yehova. Ikiwa ni hivyo, usali ili upate nguvu ya kuelezea wengine waziwazi sababu gani haujiingize katika mambo ya politike. Unaweza kuwa hakika kwamba Yehova atakusaidia uvumilie.—Soma Matendo 4:27-31.

Ujifunze maandiko ya Biblia yenye itakusaidia usijiingize katika mambo ya politike na maandiko yenye kuzungumuzia dunia mupya

15. Namna gani Biblia inaweza kutusaidia tuepuke kujiingiza katika mambo ya politike? (Soma pia kisanduku “ Neno la Mungu Liliwasaidia Wakuwe na Imani Yenye Nguvu.”)

15 Yehova ametupatia Biblia ili itutie nguvu. Ufikiri sana juu ya maandiko yenye itakusaidia uepuke kujiingiza katika mambo ya politike. Ujikaze kujifunza maandiko hayo na kuyaweka katika akili, kwa sababu yatakusaidia ikiwa wakati fulani hautakuwa na Biblia. Pia, Biblia inaweza kukusaidia ukuwe na tumaini lenye nguvu katika ahadi za Mungu za wakati unaokuja. Tunapaswa kuwa na tumaini hilo ili tuvumilie mateso. (Waroma 8:25) Utafute maandiko yenye kuzungumuzia mambo yenye utapenda zaidi sana kufanya katika dunia mupya, na ujione katika dunia mupya.

MIFANO YA WATUMISHI WAAMINIFU WA YEHOVA INAWEZA KUKUSAIDIA

16 Njia ya ine ya kutusaidia tusijiingize katika mambo ya politike ni kufikiria mifano ya watumishi waaminifu wa Yehova. Watumishi wengi wa zamani hawakuogopa, na walichukua maamuzi ya muzuri yenye iliwasaidia wasijiingize katika mambo ya politike. Ufikirie Shadraki, Meshaki, na Abednego; vijana hao walikataa kuabudu sanamu ya serikali ya Babiloni. (Soma Danieli 3:16-18.) Habari hiyo ya Biblia inasaidia ndugu na dada wengi leo ili wasiogope na wasiabudu bendera ya inchi yao. Yesu hakujiingiza katika mambo ya politike ao mambo yenye kuletea watu migawanyiko. Alijua kama mufano wake muzuri ungesaidia wanafunzi wake. Alisema hivi: ‘Mujipe moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.’—Yohana 16:33.

17 Leo ndugu na dada zetu wengi hawajiingize katika mambo ya politike. Wamoja kati yao wameteswa sana, wamefungwa, na kuuawa kwa sababu walibakia waaminifu kwa Yehova. Mifano yao inaweza kutusaidia tusiogope. Ndugu mumoja wa inchi ya Uturuki alisema hivi: “Franz Reiter alikuwa ndugu kijana mwenye aliuawa kwa sababu ya kukataa kuingia katika jeshi la Hitler. Barua yenye aliandikia mama yake usiku mbele auawe ilionyesha imani yake yenye kushangaza sana na tumaini lake kwa Yehova, na nilipenda kuiga mufano wake ikiwa ninajikuta katika hali kamahiyo.” [2]—Soma maelezo kwenye mwisho wa habari hii.

18Ndugu na dada katika kutaniko lako wanaweza kukusaidia ili usijiingize katika mambo ya politike. Ujulishe wazee ikiwa unajikuta katika hali ngumu. Wanaweza kukutolea mashauri ya muzuri kwa kutumia Biblia. Pia, ndugu na dada katika kutaniko wanaweza kukusaidia ikiwa wanajua magumu yako. Uwaambie wasali juu yako. Lakini sisi pia tunapaswa kutegemeza ndugu na dada zetu na kusali kwa ajili yao. (Mathayo 7:12) Adresi yetu ya Internete jw.org inatutolea majina ya ndugu na dada wenye wamefungwa katika gereza; unaweza kupata majina hayo kwa kufungua kichwa HABARI—MAMBO YA KISHERIA > “Mashahidi wa Yehova Walio Gerezani kwa Sababu ya Imani yao—Kulingana na Eneo.” Uchague majina fulani, na umuombe Yehova asaidie ndugu na dada hao wasiogope na wabakie waaminifu kwake.—Waefeso 6:19, 20.

18, 19. (a) Namna gani ndugu na dada katika kutaniko lako wanaweza kukusaidia uepuke kujiingiza katika mambo ya politike? (b) Unaazimia kufanya nini?

19 Kwa sababu tunakaribia mwisho wa ulimwengu huu, tunapaswa kujua kama serikali zitaendelea kutukaza sana ili tujiingize katika mambo ya politike. Ndiyo sababu tunapaswa kujitayarisha tangu leo ili tusijiingize katika mambo ya politike ya ulimwengu huu wenye kugawanyika!

^ [1] (fungu la 1) Wakati Yesu alitaja Kaisari, alikuwa anazungumuzia serikali za wanadamu. Wakati huo, Kaisari alikuwa mutawala na ndiye alikuwa mwanadamu mwenye mamlaka makubwa zaidi.

^ [2] (fungu la 17) Soma kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu, ukurasa wa 662, na kisanduku “Alikufa ili Kumuletea Mungu Utukufu” katika sura ya 14 katika kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala!