Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakristo Wanapaswa Kuabudu Kwenye Nafasi Zenye Kuonwa Kuwa Takatifu?

Wakristo Wanapaswa Kuabudu Kwenye Nafasi Zenye Kuonwa Kuwa Takatifu?

Mwaka, watu zaidi ya milioni sita wanafanya safari ya kuenda katika pori la miti ya mierezi lenye kupatikana katika eneo la Shima, inchi ya Japani. Wanakuja kwenye Nafasi Kubwa Takatifu ya Ise, ambapo Amaterasu Omikami, mungu jua mwanamuke wa dini ya Shinto ameabudiwa kwa miaka 2 000 hivi. Kwanza, waabudu hao wanajitakasa kwa kunawa mikono yao na kinywa. Kisha, wanasimama mbele ya Haiden (jumba la ibada), na wanafanya desturi yao ya kuinama, kupiga mikono, na kusali mungu wao mwanamuke. * Dini ya Shinto inaruhusu waamini wake kufanya desturi za dini zingine. Kwa hiyo, Wabuda fulani, watu wenye kujiita kuwa Wakristo, na watu wengine wanaona kama hakuna shida kufanya ibada ya dini ya Shinto nafasi hiyo yenye kuonwa kuwa takatifu.

Dini nyingi kubwa-kubwa za ulimwengu ziko na nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu, * na watu wengi sana wanaenda kutembelea nafasi hizo. Katika inchi zenye kujiita kuwa za Kikristo, kuko kanisa na nafasi nyingi zenye kuonwa kuwa takatifu kwenye watu wanaabudu Yesu, Maria, na watakatifu. Nafasi zingine kama hizo zinapatikana mahali matukio fulani ya Biblia yalitendeka ao mahali penye inasemekana kulifanyika “miujiza” ya hivi karibuni ao mahali vitu vya dini vya zamani vinawekwa. Watu wengi wanaenda kwenye nafasi hizo kwa sababu wanaamini kama sala zao zinaweza zaidi kusikiwa ikiwa zinatolewa huko. Wengine wanafikiri kama kufika kwenye nafasi takatifu ndio mwisho wa safari yao ndefu yenye wamefanya ili kuonyesha kama wanajitoa katika imani ya dini.

Watu wenye kutembelea Nafasi Kubwa Takatifu ya Ise katika inchi ya Japani, na Pango la Massabielle katika muji wa Lourdes, Ufaransa

Sala na maombi yenye kutolewa kwenye nafasi yenye kuonwa kuwa takatifu ndiyo yanasikiwa na kujibiwa? Mungu anapendezwa na roho ya kujitoa ya wale wenye kufanya safari ili kuenda kwenye nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu? Na jambo la maana zaidi, Wakristo wanapaswa kuabudu kwenye nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu? Majibu ya maulizo hayo yatatusaidia kujua namna tunapaswa kuona nafasi hizo na pia yatatusaidia kuelewa aina ya ibada yenye kupendeza Mungu.

KUABUDU KWA “ROHO NA KWELI”

Yesu alimaanisha nini wakati alisema kama tunapaswa kuabudu “kwa roho na kweli”?

Mazungumuzo kati ya Yesu na mwanamuke Musamaria yanaonyesha mawazo ya Mungu juu ya kuabudu kwenye nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu. Yesu alikuwa katika Samaria na alisimama ili kupumuzika kidogo kwenye kisima chenye kilikuwa karibu na muji wa Sikari. Alianzisha mazungumuzo pamoja na mwanamuke mwenye alikuja kushota maji kwenye kisima. Wakati waliendelea kuzungumuza, mwanamuke huyo alionyesha tofauti kubwa ya dini kati ya Wayahudi na Wasamaria. Alisema hivi: ‘Mababu [wazazi wa zamani] zetu waliabudu katika mulima huu; lakini ninyi munasema kwamba Yerusalemu ndipo mahali ambapo watu wanapaswa kuabudia.’—Yohana 4:5-9,20.

Mulima wenye mwanamuke huyo alizungumuzia ni Mulima Gerizimu, wenye ulikuwa kilometre 50 kaskazini mwa Yerusalemu. Wakati fulani Wasamaria walikuwa na hekalu huko kwenye walifanya sikukuu mbalimbali kama vile Pasaka. Lakini, kuliko kukazia tofauti hiyo kubwa, Yesu alimuambia mwanamuke huyo hivi: ‘Uniamini mimi, mwanamuke, saa inakuja wakati ambapo mutamuabudu Baba si katika mulima huu wala kule Yerusalemu.’ (Yohana 4:21) Maneno hayo yalikuwa ya kushangaza kabisa, zaidi sana kwa sababu yalisemwa na Muyahudi! Sababu gani ibada yenye ilifanywa kwenye hekalu la Yerusalemu ingeisha?

Yesu aliendelea kusema hivi: ‘Saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamuabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamuabudu.’ (Yohana 4:23) Kwa mamia ya miaka, Wayahudi waliona hekalu hilo la muzuri la Yerusalemu kuwa nafasi yao kubwa ya ibada. Walifanya safari mara tatu kila mwaka ili kuenda kumutolea zabihu Mungu wao Yehova. (Kutoka 23:14-17) Lakini Yesu alisema kama yote hayo yangebadilika na kama “waabudu wa kweli” wangeabudu “kwa roho na kweli.”

Hekalu la Wayahudi lilikuwa jengo lenye kuonekana na lilikuwa mahali fulani. Lakini roho na kweli haviwezi kuonekana, na hata haviwezi kuwa mahali fulani. Kwa hiyo, Yesu alikuwa anafasiria kama ibada ya kweli ya Kikristo haingetolewa kwenye nafasi fulani ya kimwili, ikuwe kwenye Mulima Gerizimu, hekalu la Yerusalemu, ao nafasi ingine ya ibada yenye kuonwa kuwa takatifu.

Katika mazungumuzo pamoja na mwanamuke Musamaria, Yesu alionyesha pia kama “saa inakuja” juu ya mabadiliko katika ibada ya Mungu. Saa hiyo ingefika wakati gani? Ilifika wakati Yesu, kupitia kifo chake cha zabihu, alimaliza njia ya kuabudu ya Wayahudi yenye ilitegemea Sheria ya Musa. (Waroma 10:4) Lakini, Yesu alisema tena hivi: “Saa . . . ipo sasa.” Sababu gani? Kwa sababu yeye alikuwa Masiya, na tayari alikuwa anakusanya wanafunzi wenye wangetii amri hii yenye alitoa kisha hapo: ‘Mungu ni Roho, na wale wanaomuabudu lazima wamuabudu kwa roho na kweli.’ (Yohana 4:24) Sasa, inamaanisha nini kuabudu kwa roho na kweli?

Wakati Yesu alikuwa anasema juu ya kuabudu kwa roho, hakukuwa anazungumuza juu ya kuabudu kwa motomoto ao kwa bidii sana. Lakini, alikuwa anazungumuza juu ya kuongozwa na roho takatifu ya Mungu, ambayo ni kati ya mambo yenye kutusaidia kuelewa Maandiko. (1 Wakorintho 2:9-12) Na kweli yenye Yesu alizungumuzia ni ujuzi wa kweli wa mafundisho ya Biblia. Kwa hiyo, kuliko kufanya ibada yetu kwenye nafasi fulani ya pekee, ibada yetu itakubaliwa na Mungu kama inapatana na mambo Biblia inafundisha na kama inaongozwa na roho takatifu.

MAWAZO YA WAKRISTO JUU YA NAFASI ZENYE KUONWA KUWA TAKATIFU

Sasa, namna gani Wakristo wanapaswa kuona safari za kuenda kwenye nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu ao kuabudu kwenye nafasi hizo? Kupatana na amri ya Yesu ya kwamba waabudu wa kweli wanapaswa kuabudu Mungu kwa roho na kweli, ni wazi kama ibada yenye kufanywa kwenye nafasi yoyote yenye kuonwa kuwa takatifu haina maana kwa Baba yetu wa mbinguni. Tena, Biblia inatuonyesha mawazo ya Mungu juu ya kutumia sanamu katika ibada. Inasema hivi: ‘Mukimbie ibada ya sanamu’ na ‘mujilinde na sanamu.’ (1 Wakorintho 10:14; 1 Yohana 5:21) Ni wazi kama, Mukristo wa kweli hapaswi kuabudu kwenye nafasi yoyote yenye kuonwa kuwa takatifu ao yenye kuunga mukono ibada ya sanamu. Kwa hiyo, kwa sababu wanajua ukweli juu ya nafasi zenye kuonwa kuwa takatifu, Wakristo wa kweli hawafanye ibada yao kwenye nafasi hizo.

Lakini, hilo halimaanishe kama Neno la Mungu linakataza kuwa na nafasi fulani juu ya kusali, kujifunza, ao kufikiri sana. Nafasi ya kukusanyikia yenye kupangwa muzuri na yenye kuheshimika inatuwezesha kujifunza na kuzungumuza juu ya mambo ya kiroho. Na haiko mubaya kujenga kitu fulani, kama vile kaburi, ili kukumbuka mupendwa wetu mwenye amekufa. Kufanya vile inaweza kuwa njia tu ya kukumbuka mutu huyo ao kumuonyesha upendo. Lakini, kuona nafasi hiyo kuwa takatifu, ao kuabudu sanamu ao vitu fulani vya zamani kwenye nafasi hiyo kunapingana sana na maneno ya Yesu.

Kwa hiyo, hakuna lazima ya kuenda kwenye nafasi yenye kuonwa kuwa takatifu ili Mungu asikilize sala zako. Na Mungu hatakufurahia ao kukupatia baraka za pekee kwa sababu ulifanya safari ya kuenda kwenye nafasi yenye kuonwa kuwa takatifu. Biblia inatuambia kama Yehova Mungu ‘Bwana wa mbingu na dunia, hakae katika mahekalu yaliyofanywa kwa mikono.’ Lakini, hilo halimufanye Mungu akuwe mbali na sisi. Tunaweza kusali kwake na kusikiwa nafasi yoyote kwenye tunapatikana kwa sababu yeye ‘hayuko mbali sana na kila mumoja.’—Matendo 17:24-27.

^ fu. 2 Desturi zinaweza kuwa tofauti kwenye nafasi mbalimbali za Washinto zenye kuonwa kuwa takatifu.