Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuige Mufano wa Yesu wa Kuendelea Kukesha

Tuige Mufano wa Yesu wa Kuendelea Kukesha

Tuige Mufano wa Yesu wa Kuendelea Kukesha

“Endeleeni kukesha na kusali.”​—MT. 26:41.

WEWE UNGEJIBU NAMNA GANI?

Namna gani sala zetu zinaweza kuonyesha kwamba tunaendelea kukesha?

Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunaendelea kukesha kuhusiana na kazi ya kuhubiri?

Kwa nini ni lazima tuendelee kukesha tunapokuwa katika majaribu, na tunaweza kufanya hivyo namna gani?

1, 2. (a) Ni maulizo gani mutu anaweza kujiuliza kuhusiana na mufano wa Yesu wa kuendelea kukesha? (b) Je, wanadamu wenye zambi wanaweza kujifunza kutokana na mufano mukamilifu wa Yesu? Toa mufano.

 LABDA unaweza kujiuliza hivi: ‘Kwa kuwa Yesu alikuwa mukamilifu, je, inawezekana kabisa kuendelea kukesha kama yeye? Zaidi ya hilo, nyakati fulani, Yesu alikuwa na uwezo wa kujua vizuri mambo yatakayotokea, hata maelfu ya miaka mbele! Je, alihitaji kabisa kuendelea kukesha?’ (Mt. 24:37-39; Ebr. 4:15) Acheni tuzungumuzie kwanza maulizo hayo ili tuelewe kwa nini kuendelea kukesha ni jambo la maana na la kutenda kwa haraka.

2 Je, wanadamu wasio wakamilifu wanaweza kujifunza kutokana na mutu mukamilifu? Ndiyo, ni kama vile mutu anaweza kujifunza kutokana na mwalimu muzuri na kupitia mufano wake. Kwa mufano, fikiria mutu anayejifunza kutupa mushale. Kwa mara ya kwanza, hawezi kutupa mushale na kufikia shabaha, lakini itamuomba ajifunze zaidi na kuendelea kufanya mazoezi. Ili kufanya vizuri zaidi, anajifunza kwa uangalifu mufano wa mwalimu wake, ambaye ni fundi. Mwanafunzi anatazama kwa uangalifu jinsi mwalimu anavyosimama, jinsi anavyoshika upinde, na jinsi anavyotia vidole kwenye kamba ya upinde. Polepole, mwanafunzi huyo asiye na ufundi anajifunza jinsi ya kutupa mushale, anaangalia mahali upepo unapoenda, na anaendelea kujikaza. Kwa kumwiga mwalimu wake, mwishowe anatupa mishale yake hivi kwamba inaanza kukaribia shabaha yake. Sisi pia, tunaendelea kujikaza ili kuwa na sifa nzuri za Kikristo kwa kufuata maagizo ya Yesu na kuiga mufano wake mukamilifu.

3. (a) Namna gani Yesu alionyesha kwamba alihitaji kuendelea kukesha? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Basi, tuseme nini kuhusu kuendelea kukesha? Je, kwa kweli Yesu alihitaji kuendelea kukesha? Bila shaka. Kwa mufano, usiku wa mwisho wa maisha yake hapa duniani, Yesu aliwasihi mitume wake waaminifu hivi: ‘Mwendelee kukesha pamoja nami. Mwendelee kukesha na kusali sikuzote, ili musiingie katika jaribu.’ (Mt. 26:38, 41) Sikuzote Yesu alikuwa mwenye kukesha, katika nyakati ngumu kama hizo, Yesu alitaka kuendelea kukesha zaidi, na kuwa karibu sana na Baba yake wa mbinguni. Alijua kwamba wafuasi wake walihitaji pia kukesha, si wakati huo tu lakini pia wakati ujao. Kwa hiyo, acheni tuone kwa nini Yesu anataka tuendelee kukesha. Kisha, tutajifunza njia tatu ambazo kupitia hizo tunaweza kuiga mufano wa Yesu wa kukesha katika maisha yetu ya kila siku.

KWA NINI YESU ANATAKA TUENDELEE KUKESHA

4. Namna gani kutojua mambo fulani kuhusu wakati ujao kunatuchochea tuendelee kukesha?

4 Kwa kifupi, Yesu anataka tuendelee kukesha kwa sababu ya mambo ambayo hatujui na yale tunayojua. Yesu alipokuwa duniani, je, alijua mambo yote ya wakati ujao? Hapana, yeye mwenyewe alisema hivi: ‘Kuhusu siku ile na saa ile hakuna mutu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Baba tu.’ (Mt. 24:36) Wakati huo, Yesu, “Mwana,” hakujua kabisa siku ule mwisho wa ulimwengu huu mwovu ungekuja. Namna gani sisi leo? Je, tunajua mambo yatakayotokea kesho? Hapana! Hatujue siku ambayo Yehova atamutuma Mwana wake kuharibu ulimwengu huu mwovu. Ikiwa tungejua siku hiyo, je, tungehitaji kuendelea kukesha? Kama Yesu alivyoeleza, mwisho utakuja kwa gafula, bila kutazamia; kwa hiyo tunahitaji kuendelea kukesha.​—Soma Mathayo 24:43.

5, 6. (a) Namna gani kujua mambo yatakayofanyika wakati ujao kunatusaidia kukesha? (b) Kwa nini kujua makusudi ya Shetani kunatuchochea sana kuendelea kukesha?

5 Kwa upande mwingine, Yesu alijua kabisa mambo mengi mazuri yatakayofanyika wakati ujao​—mambo ambayo watu wengine wakati huo hawakujua. Ujuzi wetu ni mudogo sana kwa kuulinganisha na ule wa Yesu, lakini kupitia Yesu tunajua mambo mengi kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo ambayo Ufalme huo utatimiza hivi karibuni. Watu tunaokutana nao, iwe kwenye masomo, kazini, ao katika mahubiri, wanaishi katika giza na hawajui mambo hayo ya ajabu, sivyo? Basi hiyo ni sababu nyingine inayotuchochea kukesha. Kama Yesu, ni lazima tuwe macho kila wakati, tusipoteze nafasi inayojitokeza ili kujulisha wengine kuhusu Ufalme wa Mungu. Kila nafasi kama hiyo inayojitokeza ni ya maana sana, na hatutaki kuipoteza. Maisha ya watu yako katika hatari!​—1 Tim. 4:16.

6 Yesu alijua jambo lingine ambalo lilimuchochea aendelee kukesha. Alijua kwamba Shetani alikusudia sana kumushawishi, kumutesa, na kumufanya avunje ushikamanifu wake. Adui huyo mwovu alingojea “wakati mwingine unaofaa” ili kumujaribu Yesu. (Luka 4:13) Yesu aliendelea kukesha. Alitaka awe tayari kwa ajili ya kila jaribu, iwe kishawishi, upinzani, ao mateso. Sisi pia tunakutana na hali kama hizo, sivyo? Tunajua kwamba Shetani angali anatenda ‘kama simba anayenguruma, akitafuta kumumeza mutu.’ Kwa hiyo, Neno la Mungu linatushauria hivi: “Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda.” (1 Pet. 5:8) Basi, namna gani tunaweza kufanya hivyo?

JINSI SALA INAVYOTUSAIDIA KUKESHA

7, 8. Yesu alitoa shauri gani kuhusu sala, na alituachia mufano gani?

7 Biblia inaonyesha kwamba ili kukaa macho kiroho, ao kukesha, ni lazima sana kusali. (Kol. 4:2; 1 Pet. 4:7) Muda kidogo mbele ya kuwaomba wafuasi wake waendelee kukesha pamoja naye, Yesu alisema: ‘Endeleeni kukesha na kusali sikuzote, ili musiingie katika jaribu.’ (Mt. 26:41) Je, Yesu alimaanisha kwamba wangeendelea kusali tu wakati wa hali ngumu ambayo walikuwa wakipambana nayo wakati huo? Hapana, shauri lake ni kanuni tunayopaswa kutumia katika maisha yetu ya kila siku.

8 Yesu alituachia mufano muzuri kuhusiana na sala. Labda unakumbuka kwamba siku moja alipitisha usiku wote akisali kwa Baba yake. Acheni tufikirie akilini kipindi hicho. (Soma Luka 6:12, 13.) Labda Yesu yuko karibu na muji wa wavua-samaki, huko Kapernaumu. Wakati wa mangaribi, Yesu anapanda milimani, huko mutu anaweza kuona vizuri Bahari ya Galilaya. Katika giza, labda anatazama kwa mbali miangaza ya taa katika Kapernaumu na vijiji vingine vilivyo karibu na muji huo. Hata hivyo, Yesu anaanza kusali, na hakuna kitu kinachomukengeusha anapozungumuza na Yehova. Dakika zinapita, kisha saa zinapita. Anaona kwamba taa zinaanza kuzimika ao mwezi unaanza kuingia na kusikia sauti za wanyama waliokuwa karibu karibu. Sala yake inahusu uamuzi muzito wa kuwachagua mitume 12. Fikiria Yesu, bila kukengeushwa na jambo lingine katika sala anamwelezea Baba yake mawazo na mahangaiko yake yote kuhusu kila mwanafunzi anapomusihi Yehova amuongoze na kumupatia hekima.

9. Tunaweza kujifunza nini kutokana na mufano wa Yesu wa kusali usiku kucha?

9 Tunaweza kujifunza nini kutokana na mufano wa Yesu? Je, tunajifunza kwamba tunapaswa kuchukua saa nyingi tunaposali? Sivyo, kwa kuwa, kuhusu wafuasi wake alisema hivi: ‘Bila shaka, roho inataka, lakini mwili ni zaifu.’ (Mt. 26:41) Hata hivyo, tunaweza kumuiga Yesu. Kwa mufano, je, tunazungumuza kwanza na Baba yetu wa mbinguni mbele ya kuchukua uamuzi ambao labda unatuhusu sisi, familia yetu, ao Wakristo wenzetu? Je, sala zetu zinaonyesha kwamba tunahangaikia ndugu na dada zetu? Je, tunasali kutoka moyoni kuliko kurudilia maneno yaleyale? Ona pia kwamba, Yesu alipenda sana kuwa na mazungumuzo ya kirafiki na ya kipekee pamoja na Baba yake. Katika ulimwengu wa leo, kwa sababu ya kwenda huku na huku ili kutafuta maisha, ni rahisi sana kusahau mambo ya maana zaidi. Ikiwa tunachukua wakati wa kutosha ili kutoa sala nzito na ya kipekee, tutaendelea kukaa macho kiroho. (Mt. 6:6, 7) Tutamukaribia Yehova, tukiwa tayari kufanya uhusiano wetu pamoja naye uwe wenye nguvu na kuepuka jambo lolote linaloweza kuregeza uhusiano huo.​—Zab. 25:14.

JINSI YA KUWA MACHO KUHUSIANA NA KAZI YA KUHUBIRI

10. Ni mufano gani unaotuonyesha namna Yesu alivyokuwa macho, yaani hakupoteza nafasi zilizojitokeza ili kutoa ushahidi?

10 Yesu aliendelea kuwa macho kuhusiana na kazi ambayo Yehova alimutolea. Kunaweza kuwa kazi ambayo hata akili ya mufanyakazi ikitangatanga hakutakuwa na hatari yoyote. Lakini, kazi ingine inaomba mutu kukaza akili na kuwa macho anapofanya kazi; kama vile kazi ya kuhubiri. Yesu aliendelea kuwa macho katika kazi yake, hakupoteza nafasi iliyojitokeza ili kuhubiria wengine habari njema. Kwa mufano, wakati yeye na wanafunzi wake walipofika katika muji wa Sikari kisha kutembea kwa muda murefu kuanzia asubuhi, wafuasi wake walienda kununua chakula. Yesu alibaki karibu na kisima cha maji ili kupumuzika, lakini alikuwa macho na hakupoteza nafasi ya kutoa ushahidi mwanamuke Musamaria alipokuja kushota maji. Yesu angetumia wakati huo ili kupumuzika kidogo. Labda angetafuta visababu vya kuepuka mazungumuzo. Hakufanya hivyo, alizungumuza na mwanamuke huyo na kumutolea ushahidi wenye kugusa moyo ambao ulisaidia watu wengi katika muji huo. (Yoh. 4:4-26, 39-42) Je, tunaweza kuiga kabisa mufano wa Yesu wa kukesha, labda kwa kujikaza kuwa macho zaidi ili tusipoteze nafasi zinazojitokeza ili kuwahubiria watu tunaokutana nao katika shuguli zetu za kila siku?

11, 12. (a) Yesu aliwaambia nini wale waliotaka kumukengeusha katika kazi yake? (b) Ni usawaziko gani ambao Yesu alionyesha kuhusiana na kazi yake?

11 Nyakati fulani, watu wenye nia nzuri walitaka kumukengeusha Yesu. Huko Kapernaumu, vikundi vya watu vilifurahishwa na miujiza ya Yesu ya kuwaponya watu hivi kwamba walitaka abaki pamoja nao. Walikuwa na sababu nzuri ya kufanya hivyo. Lakini, mugawo wa Yesu ulikuwa kuhubiri “kondoo [wote] waliopotea wa nyumba ya Israeli,” wala si watu wa muji huo tu. (Mt. 15:24) Kwa hiyo, aliwaambia watu hao hivi: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.” (Luka 4:40-44) Kwa kweli, Yesu alikazia sana akili yake kwenye kazi ya kuhubiri. Hakuruhusu jambo lolote limukengeushe.

12 Je, Yesu alishugulikia tu kazi ya kuhubiri hivi kwamba alikosa usawaziko ao kuwa mutu asiyefurahi pamoja na wengine? Je, alikuwa tu katika mahubiri hivi kwamba hakuhangaikia mahitaji ya watu? Hapana, Yesu alikuwa mufano mukamilifu wa usawaziko. Alifurahia maisha pamoja na marafiki wake. Alipendezwa na familia, alifikiria sana mahitaji na matatizo yao, na alionyesha kabisa kwamba anawapenda watoto.​—Soma Marko 10:13-16.

13. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yesu wa kukesha na wakati uleule kuwa na usawaziko kuhusiana na kazi yetu ya kuhubiri Ufalme?

13 Tunapoendelea kuiga mufano wa Yesu wa kukesha, namna gani tunaweza kuonyesha usawaziko kama yeye? Hatutaki kuruhusu ulimwengu huu utukengeushe. Hata marafiki na watu wa familia wenye nia nzuri wanaweza kutushauri tusihubiri sana ao tutafute kuwa na maisha kama watu wengine. Lakini, tukimuiga Yesu, tutaona kazi yetu ya kuhubiri kama chakula. (Yoh. 4:34) Kazi yetu inatusaidia kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova na inatuletea furaha. Lakini, hatutaki hata kidogo kuwa watu wenye kukosa usawaziko na wasiopenda kufurahia maisha pamoja na wengine. Kama Yesu, tunapenda kuwa watu wenye furaha na wenye usawaziko, watumishi wa “Mungu mwenye furaha.”​—1 Tim. 1:11.

JINSI YA KUKESHA WAKATI WA MAJARIBU

14. Wakati wa majaribu, tunapaswa kuepuka mwelekeo gani, na kwa nini?

14 Kama tulivyoona, maneno fulani ya Yesu ya maana zaidi kuhusu kuendelea kukesha, aliyasema alipokuwa katika majaribu makali. (Soma Marko 14:37.) Tunapopambana na hali ngumu, ndio wakati tunahitaji sana kufuata mufano wake. Wanapojaribiwa, watu wengi wana mwelekeo wa kusahau kweli hii ya maana inayopatikana mara mbili katika kitabu cha Methali: “Kuna njia ambayo imenyooka mbele ya mwanadamu, lakini njia za kifo ndizo mwisho wake baadaye.” (Met. 14:12; 16:25) Ikiwa tunategemea mawazo yetu, zaidi sana tunapopambana na matatizo makali, tunaweza kujitia katika hatari na kutia pia wale tunaopenda katika hatari.

15. Baba wa familia anaweza kupata jaribu gani wakati ana matatizo ya kupata feza?

15 Kwa mufano, baba wa familia anaweza kupambana na mikazo anapojikaza kutafutia “wale walio wake mwenyewe” mahitaji ya kimwili. (1 Tim. 5:8) Anaweza kushawishiwa kukubali kazi ambayo itamufanya akose mara kwa mara mikutano ya Kikristo, akose kuongoza ibada ya familia, ao akose kushiriki katika mahubiri. Ikiwa anategemea tu mawazo ya kibinadamu, uamuzi kama huo unaweza kuoneka kuwa wenye kueleweka na wenye kufaa. Lakini, uamuzi huo unaweza kumufanya aregee kiroho, ao hata kufa kiroho. Ni vizuri kabisa kufuata shauri lililo kwenye Methali 3:5, 6! Sulemani alisema hivi: ‘Mutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.’

16. (a) Yesu alituachia mufano gani wa kutegemea hekima ya Yehova kuliko kutegemea hekima yake? (b) Namna gani baba wengi wa familia wanafuata mufano wa Yesu wa kumutegemea Yehova wakati wa taabu?

16 Yesu alipokuwa katika majaribu, aliepuka kabisa kutegemea uelewaji wake. Fikiria jambo hili! Yeye aliye mutu mwenye hekima zaidi aliyepata kuishi duniani hakutegemea akili yake. Kwa mufano, Shetani alipomujaribu, Yesu alijibu kwa kurudilia maneno haya: “Imeandikwa.” (Mt. 4:4, 7, 10) Yeye alitegemea hekima ya Baba yake ili kushinda kishawishi, hivyo alionyesha unyenyekevu, sifa ambayo Shetani anakosa kabisa na ambayo anazarau. Je, sisi tunamuiga Yesu? Baba wa familia anayeiga mufano wa Yesu wa kukesha anajiacha aongozwe na Neno la Mungu, zaidi sana wakati wa taabu. Ulimwenguni pote, baba wengi wa familia wanafanya hivyo. Kwa uaminifu, wanatia faida za Ufalme na ibada ya kweli pa nafasi ya kwanza maishani na kutia mahangaiko ya kimwili pa nafasi ya pili. Kwa hiyo, wanashugulikia vizuri zaidi familia zao. Yehova anabariki jitihada zao kwa kuwapatia mahitaji yao ya kimwili kama anavyoahidi katika Neno lake.​—Mt. 6:33.

17. Ni nini kinachotusaidia ili tuendelee kuiga mufano wa Yesu wa kukesha?

17 Bila shaka, Yesu alituachia mufano muzuri zaidi wa kuendelea kukesha. Mufano wake ni wenye kufaa, wenye kusaidia, na hata wenye kuokoa uzima. Kumbuka kwamba Shetani anafanya nguvu yake yote ili kukufanya ulale kiroho, yaani, uregee katika imani, umwabudu Mungu kijuujuu, na usiwe mushikamanifu. (1 The. 5:6) Usimuruhusu ashinde! Endelea kukesha kama Yesu. Tatafuta wakati wa kusali, kesha kuhusiana na kazi ya kuhubiri na umutegemee Yehova wakati wa majaribu. Kwa kufanya hivyo, hata sasa utakuwa na maisha yenye baraka, furaha, na yenye kutosheleza kadiri unavyoona ulimwengu huu mwovu unavyozimia. Ukiendelea kukesha, Bwana wetu anapofika kuharibu ulimwengu huu, atakukuta macho na mwenye bidii ukifanya mapenzi ya Baba yake. Yehova atafurahi kabisa kukubariki kwa sababu ya uaminifu wako!​—Ufu. 16:15.

[Maulizo ya Funzo]

[Picha katika ukurasa wa 6]

Yesu alihubiria mwanamuke kwenye kisima. Ni nafasi gani zinazojitokeza kwako kila siku?

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kutosheleza mahitaji ya kiroho ya familia yako kunaonyesha kwamba unaendelea kukesha