Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hii “Ndiyo Njia Iliyokubaliwa Nawe”

Hii “Ndiyo Njia Iliyokubaliwa Nawe”

“Umewaficha kwa uangalifu wenye hekima na walio na akili mambo hayo, nawe umeyafunua kwa watoto.”LU. 10:21.

1. Ni nini ilimufanya Yesu ‘akuwe na shangwe sana katika roho takatifu’? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

WAZIA namna mambo yalikuwa wakati Yesu Kristo ‘alikuwa na shangwe [furaha] sana katika roho takatifu’! Pengine unaona namna sura na macho yake vinaonyesha furaha kubwa. Ni nini ilimufanya akuwe na furaha hiyo? Alikuwa ametoka tu kuwatuma wanafunzi 70 ili waende kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Alipendezwa sana na namna wangetimiza kazi yao. Kulikuwa maadui wengi wenye uwezo, kama vile waandishi na Mafarisayo ambao walikuwa na akili na elimu ya hali ya juu sana. Maadui hao hawakupenda habari njema ihubiriwe. Waliwachochea watu wengi wamuone Yesu kuwa seremala tu, na waone wanafunzi wake kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” (Mdo. 4:13; Mk. 6:3) Hata hivyo, wanafunzi wake walirudia katika kazi yao wakiwa na furaha kubwa sana. Walihubiri habari njema hata kama kulikuwa roho waovu na watu wenye kuwapinga! Ni nini ilifanya wakuwe wenye furaha na wenye bidii?—Soma Luka 10:1, 17-21.

2. (a) Ni katika njia gani wanafunzi wa Yesu walikuwa kama watoto? (b) Ni nini ilisaidia wafuasi wa Kristo waelewe mafundisho mazito ya maana sana?

2 Ona maneno yenye Yesu alimuambia Yehova: ‘Ninakusifu wewe hazarani [mbele ya watu], Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye akili na umeyafunua kwa watoto. Ndiyo, Ee Baba, kwa sababu kufanya hivyo kulikuwa ndiyo njia iliyokubaliwa nawe.’ (Mt. 11:25, 26) Bila shaka, Yesu hakutaka kumaanisha kwamba wanafunzi wake walikuwa watoto kabisa. Lakini, alijua kwamba walikuwa kama watoto kwa kulinganishwa na watu wenye akili na elimu ya juu sana, watu wenye walijiona kuwa wenye hekima. Zaidi ya hilo, Yesu alifundisha wafuasi wake wakuwe kama watoto, ni kusema, waendelee kuwa wanyenyekevu na kuwa tayari kukubali mafundisho. (Mt. 18:1-4) Unyenyekevu huo uliwaletea faida gani? Kupitia roho yake takatifu, Yehova aliwasaidia waelewe mafundisho mazito ya maana sana. Lakini watu wenye hekima na akili wenye walizarau mafundisho hayo, waliendelea kupofushwa na Shetani na kiburi chao wenyewe.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Yesu alikuwa na sababu ya kuwa na furaha kabisa. Jambo lenye lilimufurahisha ni kuona namna Yehova alifunua mafundisho mazito kwa watu wapole ao wanyenyekevu wa namna zote, hata kama hawakusoma mingi ao kuwa na akili nyingi. Alifurahi kuona kwamba hiyo ndiyo njia ya kufundisha yenye kukubaliwa na Baba yake. Kwa sababu Yehova hajabadilika, ni nini inaonyesha kwamba angali anakubali njia hiyo ya kufundisha? Katika habari hii, tutachunguza namna Yehova anafunua mafundisho mazito kwa watu wanyenyekevu leo.

WATU WA KILA NAMNA WANAELEWA MAFUNDISHO MAZITO

4. Ni katika njia gani gazeti Munara wa Mulinzi katika luga rahisi ni zawadi yenye kuonyesha upendo?

4 Katika miaka ya hivi karibuni, tengenezo la Yehova limekazia sana mafundisho ya kiroho yenye kuwa wazi na mwepesi zaidi. Tufikirie mifano tatu. Kwanza, tuko na gazeti la funzo la Munara wa Mulinzi katika luga rahisi. * Watu wenye kuwa na magumu ya kusema ao kusoma luga fulani, wameona kwamba gazeti hilo ni zawadi yenye kuonyesha upendo. Baba wa familia wameona kwamba sasa watoto wao wanatoa sana maelezo wakati wa funzo la Munara wa Mulinzi, njia kubwa yenye mutumwa mwaminifu anatumia ili kututolea chakula cha kiroho. Wakristo wengi wameandikia Baraza Linaloongoza maneno yenye kugusa moyo ili kuonyesha shukrani yao. Kwa mufano, dada mumoja aliandika kwamba alikuwa anasita kutoa maelezo wakati wa Funzo la Munara wa Mulinzi. Alisema hivi: “Nilikuwa ninasikia haya sana.” Lakini leo hasikie tena haya! Kisha kuanza kutumia gazeti lenye kuwa katika luga rahisi, aliandika hivi: “Leo siogope tena, ninatoa maelezo zaidi ya mara moja! Ninamushukuru Yehova na ninyi pia.”

5. Taja faida fulani za Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa.

5 Pili, tuko na Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa. Tafsiri hiyo ilitolewa katika Kiingereza kwenye mukutano wa kila mwaka wenye ulifanyika tarehe 5 Mwezi wa 10, 2013. * Katika Biblia hiyo, maandiko mengi yanatumia sasa maneno madogo, lakini maana yake inabakia ileile na inakuwa wazi zaidi. Kwa mufano, andiko la Ayubu 10:1 lilikuwa na maneno 27, lakini Biblia ya sasa ya Kiingereza inatumia maneno 19. Pia andiko la Methali 8:6 lilikuwa na maneno 20, lakini sasa lina maneno 13. Maandiko hayo mawili, iko wazi zaidi katika Biblia hiyo ya sasa. Mukristo mumoja mutiwa-mafuta mwenye ametumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi alisema hivi: “Nimemaliza tu kusoma kitabu cha Ayubu katika Biblia ya sasa, lakini ninajisikia kama vile nimekielewa kwa mara ya kwanza!” Wakristo wengi wamesema kama yeye.

6. Unajisikia namna gani kuhusu mafasirio mapya ya andiko la Mathayo 24:45-47?

6 Tatu, tufikirie mafasirio mapya ya hivi karibuni ya mafundisho yetu. Kwa mufano, tulifurahia sana mafasirio mapya juu ya ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara,’ yenye ilitolewa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013. (Mt. 24:45-47) Mafasirio hayo yalionyesha kwamba mutumwa mwaminifu ni Baraza Linaloongoza, na kwamba ‘watumishi wa nyumbani’ ni wale wote wenye kulishwa chakula cha kiroho, iwe ni Wakristo watiwa-mafuta ao “kondoo wengine.” (Yoh. 10:16) Bila shaka, tunafurahi sana kujua mafundisho hayo ya kweli na kuyafundisha wapya! Ni katika njia gani zingine Yehova ameonyesha kwamba anakubali njia ya kufundisha yenye kuwa mwepesi na wazi?

HABARI ZA BIBLIA ZINAELEZWA KWA NJIA YENYE KUWA MWEPESI NA WAZI ZAIDI

7, 8. Taja mifano yenye kuongozwa na roho ya Mungu ambayo inafananisha mambo makubwa yenye ingefanyika wakati unaokuja.

7 Ikiwa umemutumikia Yehova kwa miaka mingi, pengine umejionea mabadiliko yenye imefanywa hatua kwa hatua kuhusu namna vichapo vyetu vinafasiria habari nyingi zenye kuzungumuziwa katika Biblia. Ni mabadiliko gani hayo? Zamani katika vichapo vyetu, tulizoea kutumia vifananishi na vifananishwa ili kufasiria habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia. Habari fulani yenye kuzungumuziwa katika Biblia iliitwa kifananishi, na kila utimizo wa unabii wa habari hiyo uliitwa kifananishwa. Kuna sababu nzuri zenye zilituchochea tufasirie mambo hivyo? Ndiyo. Kwa mufano, Yesu alizungumuzia “ishara ya nabii Yona.” (Soma Mathayo 12:39, 40.) Yesu alisema kwamba wakati ambao Yona alifanya katika tumbo la samaki ulifananisha wakati ambao angefanya katika kaburi.

8 Biblia iko na habari nyingi zenye kuongozwa na roho ya Mungu ambazo zinafananisha mambo makubwa yenye ingefanyika wakati unaokuja. Mutume Paulo alizungumuzia habari fulani kati ya habari hizo. Kwa mufano, alizungumuzia uhusiano wa Abrahamu pamoja na Hagari na Sara, na akaonyesha kwamba uhusiano huo ulifananisha uhusiano wenye Yehova alikuwa nao pamoja na taifa la Israeli na pamoja na sehemu isiyoonekana ya tengenezo la Mungu. (Gal. 4:22-26) Pia, alizungumuzia mambo kama vile, tabenakulo na hekalu, Siku ya Upatanisho, kuhani mukubwa, na mambo mengine ya Sheria ya Musa, na akaonyesha kwamba ni “kivuli cha mambo mema yatakayokuja.” (Ebr. 9:23-25; 10:1) Kujifunza mambo kama hayo, kunafurahisha sana na kunatia nguvu imani yetu. Hata hivyo, tunaweza kusema kwamba kila mutu mwenye kuzungumuziwa katika Biblia, kila tukio, na kila kitu ni kivuli cha mutu fulani ao cha jambo fulani?

9. Habari ya Nabothi yenye kuzungumuziwa katika Biblia, ilifasiriwa namna gani zamani?

9 Zamani, vichapo vyetu vilizoea kuonyesha kwamba kila habari yenye kuzungumuziwa katika Biblia ni kivuli cha mambo makubwa yenye ingefanyika. Tuzungumuzie mufano wa Nabothi ambaye alitendewa bila haki. Malkia muovu Yezebeli alifanya mipango ya kumuua ili Ahabu, bwana yake, akamate shamba la mizabibu la Nabothi. (1 Fal. 21:1-16) Katika mwaka wa 1932, vichapo vyetu vilifasiria kwamba habari hiyo ilifananisha mambo makubwa yenye ingefanyika wakati unaokuja. Mafasirio hayo yalionyesha kwamba Ahabu na Yezebeli walifananisha Shetani na tengenezo lake; na yalionyesha pia kwamba Nabothi alifananisha Yesu; na kwamba kifo cha Nabothi kilifananisha kifo cha Yesu. Lakini kisha miaka mingi, kitabu “Que ton nom soit sanctifié” (Jina Lako Litakaswe) chenye kilitolewa katika mwaka wa 1961, kilionyesha kwamba Nabothi alifananisha Wakristo watiwa-mafuta na kwamba Yezebeli alifananisha dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Kwa hiyo, matendo yenye Yezebeli alimutendea Nabothi ilifananisha mateso yenye Wakristo watiwa-mafuta wanapata katika siku hizi za mwisho. Kwa miaka mingi, watumishi wa Mungu waliona kwamba kufasiria hivyo habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, kulitia nguvu imani yao. Hata hivyo, sababu gani mambo yamebadilika?

10. (a) Namna gani busara imemusaidia mutumwa mwaminifu akuwe mwangalifu zaidi wakati anafasiria habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia? (b) Leo, wakati vichapo vyetu vinafasiria habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, vinakazia mambo gani?

10 Kwa muda wa miaka mingi, Yehova amemusaidia ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ akuwe mwenye busara zaidi. Busara imemusaidia akuwe mwangalifu zaidi wakati anafasiria kwamba habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia, ni kivuli cha mambo makubwa yenye ingefanyika wakati unaokuja. Anafanya hivyo tu ikiwa kuna andiko fulani lenye kuonyesha wazi sababu za kufanya hivyo. Zaidi ya hilo, ilikuwa vigumu kwa watu wengi kuelewa mafasirio hayo ya zamani yenye kuhusu vifananishi na vifananishwa. Mafasirio hayo ya kutafuta kujua ni nani anafananisha nani na sababu gani, inaweza kuwa vigumu kuielewa, kuimbuka, na kuitumia katika maisha. Tena, wakati vifananishi vinakaziwa sana katika habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia, jambo hilo linaweza kupoteza mambo ya lazima yenye watu wanaweza kujifunza katika habari hizo. Kwa hiyo, leo wakati vichapo vyetu vinafasiria habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, vinafanya hivyo kwa njia mwepesi, vinakazia mambo yenye tunajifunza juu ya imani ya watu fulani, uvumilivu wao, namna walishikamana na Mungu, na vinakazia sifa zingine zenye walionyesha. *

Tunajifunza somo la maana sana katika mufano wa Nabothi(Ona fungu la 11)

11. (a) Namna gani tunaelewa leo habari juu ya Nabothi, na sababu gani mufano wake unahusu kila mumoja wetu? (b) Sababu gani vichapo vyetu havizoee tena kutumia vifananishi na vifananishwa? (Ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika gazeti hili.)

11 Namna gani tunaelewa leo habari juu ya Nabothi? Habari hiyo inaelezwa katika maneno mepesi sana na yenye kuwa wazi zaidi. Mutu huyo mwenye haki alikufa kwa sababu ya uaminifu wake, lakini si kwa sababu alifananisha Yesu ao Wakristo watiwa-mafuta. Alishikamana na Sheria ya Yehova wakati Ahabu na bibi yake walitumia mamlaka yao vibaya. (Hes. 36:7; 1 Fal. 21:3) Mufano wake unafundisha kila mumoja wetu kwamba anaweza kuteseka kwa sababu ya ushikamanifu wake kwa Yehova kama vile Nabothi. (Soma 2 Timotheo 3:12.) Watu wa namna zote wanaweza sasa kuelewa, kukumbuka, na kutumia katika maisha yao mambo yenye wamejifunza katika habari hiyo yenye kutia nguvu imani yetu.

12. (a) Tunapaswa kuepuka nini kuhusu habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia? (b) Sababu gani tunaweza kupata mafasirio yenye kuwa wazi juu ya mafundisho mazito ya Neno la Mungu? (Ona maelezo ya chini.)

12 Tunaweza kusema kwamba habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia zinaonyesha tu mambo yenye tunajifunza katika habari hizo? Hapana. Leo, vichapo vyetu vinaonyesha zaidi kwamba habari moja ya Biblia inaweza kutukumbusha habari ingine, ao inaweza kuwa mufano wa habari ingine. Vichapo vyetu havizoee tena kufasiria kwamba habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia ni vifananishi ao vifananishwa. Kwa mufano, tunaweza kusema kwamba uaminifu wa Nabothi wakati aliteswa na kuuawa, unatukumbusha uaminifu wa Kristo, na wa watiwa-mafuta wake. Lakini pia, unatukumbusha ushikamanifu wa “kondoo wengine” wa Bwana. Mafasirio hayo yenye kuwa mwepesi sana na yenye kuwa wazi, ni njia yenye Yehova anatumia ili kutufundisha leo. *

MIFANO YA YESU INAFASIRIWA KWA NJIA MWEPESI ZAIDI

13. Ni nini inaonyesha kwamba leo tunafasiria mifano fulani ya Yesu kwa njia yenye kuwa mwepesi na wazi zaidi?

13 Yesu ndiye mwalimu mukubwa zaidi kuliko watu wote wenye wameishi hapa duniani. Alipenda sana kutumia mifano wakati alikuwa anafundisha watu. (Mt. 13:34) Mifano inatusaidia kukumbuka mambo na inagusa moyo wetu. Tunaweza kusema kwamba kwa muda wa miaka mingi, vichapo vyetu vimefikia kufasiria mifano ya Yesu kwa njia yenye kuwa mwepesi na wazi zaidi? Bila shaka, jibu ni ndiyo! Tulifurahi sana wakati tulipata mafasirio mapya juu ya mufano wa Yesu kuhusu chachu, mbegu ya haradali, na wavu, ambayo ilizungumuziwa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2008. Leo tunaelewa kwamba mifano hiyo inahusu Ufalme wa Mungu na matokeo yenye kushangaza ambayo Ufalme huo unapata katika kazi ya kukusanya wafuasi wa Kristo kutoka katika ulimwengu huu wa Shetani.

14. (a) Zamani, namna gani tulikuwa tunafasiria mufano wa Musamaria mwema? (b) Namna gani tunaelewa leo mufano huo wa Yesu?

14 Tuseme nini sasa kuhusu mifano yenye kuwa na maelezo mengi yenye Yesu alitoa? Kwa kweli, mifano fulani ni ya kufananisha mambo na ingine ni ya unabii; lakini mifano ingine inakazia mambo fulani yenye tunaweza kujifunza. Tunafikia namna gani kujua hivyo? Kwa miaka mingi, mafasirio ya mifano hiyo imekuwa wazi hatua kwa hatua. Kwa mufano, tuzungumuzie namna tulikuwa tunafasiria hapo zamani mufano wa Yesu wa Musamaria mwema. (Lu. 10:30-37) Katika mwaka wa 1924, gazeti Munara wa Mulinzi lilisema kwamba Musamaria mwema alifananisha Yesu. Pia barabara ya kutoka Yerusalemu kuenda Yeriko, yenye ilikuwa ya kushuka, ilifananisha hali ya wanadamu yenye iliendelea kushuka tangu uasi wa Edeni. Na wanyanganyi wenye walikuwa katika barabara walifananisha mashirika makubwa-makubwa ya wafanya-biashara wenye kutafuta faida zao wenyewe. Kisha, likasema kwamba kuhani na Mulawi walifananisha viongozi wa dini. Leo, vichapo vyetu vinatumia mufano huo ili kutukumbusha kwamba Wakristo wote wanapaswa kuepuka ubaguzi wakati wanasaidia watu wenye kuwa na lazima ya musaada, zaidi sana katika njia ya kiroho. Bila shaka tunafurahi sana kwa sababu Yehova amefanya mafundisho yake kuwa mwepesi zaidi.

15. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

15 Katika habari yenye kufuata, tutachunguza mufano mwingine wa Yesu, ni kusema, mufano wa mabikira kumi. (Mt. 25:1-13) Namna gani Yesu alipenda wafuasi wake wenye kuishi katika siku za mwisho waelewe mufano huo wenye maana zaidi? Alipenda kutuonyesha kwamba mafasirio ya mufano huo yenye kuwa na utimizo wa mufano yanahusu kila mutu, kila jambo, ao kila tukio? Ao, alipenda wafuasi wake wajifunze somo fulani la maana lenye lingewaongoza katika siku za mwisho? Acha tuone.

^ fu. 4 Gazeti katika luga rahisi lilipatikana kwa mara ya kwanza katika Kiingereza, Mwezi wa 7, 2011. Kuanzia wakati huo gazeti hilo linapatikana katika luga zingine chache.

^ fu. 5 Matayarisho yanafanywa ili Biblia hiyo itafsiriwe katika luga zingine.

^ fu. 10 Kwa mufano, kitabu Tuige Imani Yao kinazungumuzia kwa kirefu maisha ya watu 14 wenye kuzungumuziwa katika Biblia. Habari zenye kupatikana katika kitabu hicho zinakazia mambo yenye tunajifunza kuhusu maisha ya watu hao, bila kuonyesha kifananishi ao kifananishwa.

^ fu. 12 Bila shaka, Neno la Mungu liko na mambo yenye inaweza kuonekana kuwa “magumu kuelewa,” kama vile sehemu fulani zenye kupatikana katika barua za mutume Paulo. Hata hivyo, waandikaji wote wa Biblia waliongozwa na roho takatifu. Roho hiyo inasaidia Wakristo wa kweli leo waelewe kweli zenye Yehova anatutolea na inafanya sisi wenye kuwa na akili kidogo tuelewe kwa njia yenye kuwa wazi zaidi “hata mambo mazito ya Mungu.”—2 Pet. 3:16, 17; 1 Kor. 2:10.