Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Karibuni mambo itakuwa muzuri

Karibuni mambo itakuwa muzuri

Karibuni mambo itakuwa muzuri

“Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena . . . Lakini wapole watariti dunia, na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.”​—ZABURI 37:10, 11.

UNAPENDA kuona namna ule unabii utatimia? Tunatumaini unapenda. Kuko mambo yenye kutuhakikishia kama karibuni ule unabii utatimia.

Habari zenye zilitangulia zilizungumuzia maunabii mbalimbali ya Biblia yenye inaonyesha waziwazi kama tunaishi mu “siku za mwisho.” (2 Timoteo 3:1-5) Mungu aliongoza waandikaji wa Biblia waandike ile mambo juu itupatie tumaini. (Waroma 15:4) Kutimia kwa ile maunabii kunaonyesha kama mateso yenye tuko napata leo inakaribia kuisha.

Kisha siku za mwisho, kutatokea nini? Ufalme wa Mungu utatawala wanadamu wote. (Matayo 6:9) Ona maunabii ya Biblia yenye inaonyesha namna hali itakuwa ku dunia ile wakati:

Hakutakuwa njala. “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.”​—Zaburi 72:16.

Hakutakuwa magonjwa. “Na hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’”​—Isaya 33:24.

Dunia itakuwa tena ya muzuri. “Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi, jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.”​—Isaya 35:1.

Ile ni maunabii kidogo tu yenye kutia moyo yenye itatimia karibuni. Tunakutia moyo uombe Mashahidi wa Yehova wakuonyeshe juu ya nini wanaamini kabisa kama karibuni mambo itakuwa muzuri.