Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?”

“Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?”

“Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?”

● Kutoka anga za juu, Dunia huonekana kama kito maridadi chenye rangi ya bluu na nyeupe. Lakini unapochunguza mambo kwa ukaribu, unapata kwamba dunia yetu ina matatizo. Kwa nini? Jibu ni rahisi: Wakaaji wa dunia wamekuwa wabaya. Isitoshe, wakaaji hao wanaiharibu dunia si kihalisi tu kupitia uchafuzi, ukataji wa misitu, na kutumia vibaya mali zake za asili, bali pia wanaiharibu kiadili na kiroho kupitia ujeuri, umwagaji wa damu, na mwenendo mchafu kingono.

Hali hiyo yenye kuhuzunisha ilitabiriwa miaka 2,000 hivi iliyopita katika unabii mbalimbali wenye kustaajabisha unaopatikana katika Biblia. (2 Timotheo 3:1-5; Ufunuo 11:18) Biblia pia ilitabiri kwamba Mungu ndiye atakayerekebisha mambo kikamilifu, bali si mwanadamu. Mambo hayo muhimu yatazungumziwa kwenye hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Je, Wanadamu Wataiharibu Dunia Kabisa?” Hotuba hiyo itatolewa kwenye Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova lenye kichwa, “Ufalme wa Mungu na Uje!” Kusanyiko hilo litaanza Mei (Mwezi wa 5) nchini Marekani na kuendelea katika sehemu nyingine duniani.

Unaalikwa kwa moyo mkunjufu uhudhurie kusanyiko litakalofanywa karibu na mahali unapoishi. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au waandikie barua wachapishaji wa gazeti hili. Tovuti ya www.ps8318.com ina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Malawi, Rwanda, Tanzania, na Uganda.