Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kanuni za Biblia Zingali Zenye Kufaa leo

Kanuni za Biblia Zingali Zenye Kufaa leo

Kanuni za Biblia Zingali Zenye Kufaa leo

‘Neno lako ni taa ya muguu wangu, na nuru kwa barabara yangu.’​—ZABURI 119:105.

SABABU GANI BIBLIA NI TOFAUTI NA VITABU VINGINE VYOTE? Vitabu fulani vinaweza kuonwa kuwa vitabu vilivyoandikwa na watu waliosoma sana, lakini haviwasaidie watu katika maisha. Na vitabu vya leo vya mafundisho wanavisahihisha mara kwa mara. Lakini, Biblia inasema kama “mambo yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha.”​—Waroma 15:4.

KWA MUFANO: Hata ikiwa Biblia si kitabu kinachofundisha mambo ya matunzo, ina mashauri yanayoweza kumusaidia mutu awe na afya nzuri na moyo mutulivu. Tuchukue mufano, Biblia inasema kama ‘moyo mutulivu ni uzima wa mwili.’ (Methali 14:30) Tena Biblia inasema kama ‘mutu anayejitenga na wengine atatafuta mapendezi yake mwenyewe; atashindana na hekima yote inayotumika.’ (Methali 18:1) Pia, inasema kama “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”​—Matendo 20:35.

YALE WACHUNGUZI WANASEMA: Kuwa mutulivu, kuwa na marafiki wa kweli, na kuwa mukarimu kunaweza kufanya mutu awe na afya nzuri. Gazeti moja (The Journal of the American Medical Association) linasema hivi: “Watu wanaokasirika sana wana hatari mara mbili ya kupatwa na magonjwa ya ubongo yanayofanya sehemu fulani ya mwili ipooze, kuliko wale wanaozuia kasirani yao.” Uchunguzi fulani uliofanywa kwa muda wa miaka kumi huko Australie ulionyesha kama watu waliozeeka ambao walikuwa wakizungumuza na watu wengi kwenye Internete na ambao walikuwa pia na marafiki ambao walikuwa wakizungumuza nao mambo ya siri, wanaweza kuishi kwa muda murefu. Uchunguzi mwingine ulifanywa katika mwaka wa 2008 huko Canada na États-unis. Uchunguzi huo ulionyesha pia kama “mutu anayetumia feza zake ili kusaidia watu wengine ana furaha zaidi kuliko yule anayezitumia kwa ajili yake mwenyewe.”

UNAWAZA NAMNA GANI? Unawaza kama unaweza kutumainia mashauri ya afya yaliyo katika kitabu kingine kilichoandikwa kumepita miaka karibu 2 000? Hauone kama Biblia ni tofauti kabisa na vitabu vingine?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 8]

HOWARD KELLY, MUGANGA KWENYE MASOMO YA JUU YA KIGANGA (THE JOHNS HOPKINS UNIVERSITY) alisema hivi: “Biblia inanipendeza sana . . . kwa sababu ina mashauri mazuri ya kiganga.”