Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unaweza Kuamini Miujiza Inayozungumuziwa Katika Biblia?

Je, Unaweza Kuamini Miujiza Inayozungumuziwa Katika Biblia?

Je, Unaweza Kuamini Miujiza Inayozungumuziwa Katika Biblia?

IKIWA mutu anakuambia habari fulani yenye kushangaza, utaamini habari hiyo ikiwa unajua kama mutu huyo ana tabia ya kusema kweli, sivyo? Hautaamini kwa sababu tu ya namna anavyoeleza habari hiyo, lakini pia kwa sababu anajulikana kuwa musema kweli. Ikiwa mutu huyo amekuambia kweli kwa muda wa miaka mingi na hajakudanganya hata kidogo, ni wazi kama utaamini mambo anayokuelezea.

Ni vilevile juu ya miujiza inayozungumuziwa katika Biblia. Hakuna mutu kati yetu aliyekuwa hapo wakati miujiza hiyo ilifanyika. Lakini, tunaweza kujua ikiwa mambo ambayo Biblia inasema ni yenye kutumainika na ni ya kweli. Namna gani? Tuone mambo fulani yanayofanya miujiza ambayo Biblia inazungumuzia iwe yenye kutumainika.

Miujiza mingi ilifanywa mbele ya watu wengi. Wakati fulani, watu wengi sana walikuwa hapo na waliona wakati miujiza hiyo ilifanyika. (Kutoka 14:21-31; 19:16-19) Haikufanyika kwa siri.

Miujiza hiyo haikuomba mambo mengi. Haikuomba mambo ya ajabu-ajabu wala miangaza ya kuwadanganya watu. Mara nyingi, miujiza inayozungumuziwa katika Biblia ilifanyika bila kutayarishwa na ilifanywa kupatana na mahitaji ya watu waliokuwa hapo. (Marko 5:25-29; Luka 7:11-16) Katika hali hizo, yule aliyefanya miujiza hangeipanga mbele ya wakati.

Wale waliofanya miujiza hiyo hawakuifanya ili wajulikane, watukuzwe, ao wajipatie mali. Waliifanya ili kumutukuza Mungu. (Yohana 11:1-4, 15, 40) Wale waliofanya miujiza hawakuruhusiwa kutumia uwezo wao wa kufanya miujiza ili kujitajirisha.​—2 Wafalme 5:15, 16, 20, 25-27; Matendo 8:18-23.

Miujiza inayozungumuziwa katika Biblia ni tofauti-tofauti, na hilo linaonyesha kama haingefanyika kwa nguvu za wanadamu. Kwa mufano, bahari na upepo mukali vilitulizwa, maji yaligeuzwa kuwa divai, mvua ilizuiwa kunyesha kwa muda murefu na kuanzishwa tena, wagonjwa waliponyeshwa, na vipofu waliona. Miujiza hiyo yote na mingine mingi inaonyesha kama nguvu fulani inayopita ya mwanadamu, inayoweza kutenda juu ya vitu mbalimbali, ndiyo iliwezesha miujiza kama hiyo ifanyike.​—1 Wafalme 17:1-7; 18:41-45; Mathayo 8:24-27; Luka 17:11-19; Yohana 2:1-11; 9:1-7.

Wapinzani walioona miujiza hiyo hawakuikataa. Wakati Yesu alimufufua rafiki yake Lazaro, wapinzani wa Yesu hawakukataa kama Lazaro alikuwa amekufa. Hawangeweza kukataa kwa sababu Lazaro alikuwa amezikwa kwa muda wa siku ine. (Yohana 11:45-48; 12:9-11) Hata miaka mingi kisha Yesu kufa, waandikaji wa Talmud (kitabu cha dini ya Wayahudi) waliendelea kukubali kama Yesu alikuwa na uwezo wa kufanya miujiza. Lakini jambo walilokataa ni lile la kusema kama uwezo wake wa kufanya miujiza ulitoka kwa Mungu. Vilevile, wakati wafuasi wa Yesu walipelekwa mbele ya tribinali kubwa ya Wayahudi, hawakuulizwa “Je, mulifanya muujiza?” Lakini waliulizwa hivi: ‘Mulifanya jambo hilo kwa nguvu gani ao katika jina la nani?’​—Matendo 4:1-13.

Je, unaweza sasa kuamini yale Biblia inatuambia juu ya miujiza? Kupatana na miujiza ambayo tumechunguza, ni wazi kama miujiza inayozungumuziwa katika Biblia ni yenye kutumainika kabisa. Kuna sababu zingine za kuamini miujiza ambayo Biblia inazungumuzia. Kwa mufano, wakati Biblia inazungumuzia jambo fulani, mara nyingi inatupatia wakati jambo hilo lilifanyika, mahali, na majina ya watu wanaozungumuziwa. Hata wachambuzi wa Biblia wameshangazwa na namna Biblia inavyozungumuzia mambo ya historia bila kukosea. Unabii mwingi wa Biblia umetimizwa, hata katika mambo madogo​-madogo. Tena, Biblia ina mashauri mengi yanayoonyesha namna ya kuwa na uhusiano muzuri na watu wengine​—mashauri ambayo yamesaidia watu wa kila umri, watu masikini ao matajiri. Mashauri ambayo Biblia inatoa kuhusu namna ya kuwa na uhusiano na watu wengine yanapita kabisa mashauri mengine yote.

Ikiwa hautumainie kabisa Biblia, sababu gani usichukue wakati ili uichunguze wewe mwenyewe kwa uangalifu? Kadiri unavyoijua vizuri, ndivyo utaitumainia kabisa. (Yohana 17:17) Utaona kama unaweza kutumainia yale inayosema juu ya miujiza iliyofanyika wakati wa zamani. Na unapoamini miujiza hiyo ya zamani, utaamini pia miujiza ambayo Biblia inasema kama itafanyika hivi karibuni.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Wapinzani wa Yesu hawakukataa kama Lazaro alikuwa amekufa