Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kwa Wasomaji Wetu

Kwa Wasomaji Wetu

Gazeti ambalo unasoma sasa lilianza kuchapishwa tangu Mwezi wa 7, 1879. Tangu mwaka huo, nyakati zimebadilika, na gazeti hili pia limebadilika. (Ona picha zilizo juu.) Kuanzia toleo hili, utaona mabadiliko mengine katika muundo wa Munara wa Mulinzi. Ni mabadiliko gani?

Katika inchi nyingi, watu wengi sana wanapata habari kwenye Internete na wanafurahia jambo hilo. Kwa kuingia tu kwenye Internete, wanaweza kupata habari nyingi. Unaweza pia kusoma vitabu vingi, na magazeti mbalimbali kwenye Internete.

Kwa sababu watu wengi wanapenda kusoma kwenye Internete, tulibadilisha kabisa adresi yetu ya Internete ili kuifanya iwe yenye kuvutia zaidi na nyepesi kutumia. Wale wanaosoma habari kwenye Internete wanaweza kusoma vichapo vyetu ambavyo vinapatikana katika luga zaidi ya 430. Hata hivyo, kuanzia Mwezi huu wa 1, wale wanaosoma vichapo vyetu kwenye adresi yetu ya Internete wanaweza pia kusoma habari zilizochaguliwa ambazo zilichapishwa mara kwa mara katika magazeti yetu lakini sasa zitapatikana tu kwenye adresi yetu ya Internete. *

Kwa sababu tutakuwa tunaweka habari nyingi kwenye Internete tu, kuanzia Mwezi huu wa 1, gazeti la watu wote la Munara wa Mulinzi litapunguzwa kutoka kurasa 32 mupaka kurasa 16. Kwa sasa gazeti hili linachapishwa katika luga 204. Kwa sababu litakuwa na kurasa chache, linaweza sasa kutafsiriwa katika luga nyingi zaidi.

Tunatumaini kwamba mabadiliko hayo yatatuwezesha kuwahubiria watu wengi zaidi ujumbe wa Biblia wenye kuokoa uzima. Tunaazimia kuendelea kuwapa watu habari nyingi zenye kuelimisha na kuvutia, iwe ni habari zilizochapishwa ao zinazopatikana kwenye Internete. Kusudi letu ni kuwafaidi wasomaji wetu wengi ambao wanaiheshimu Biblia na wanaopenda kujua yale ambayo Biblia inafundisha kabisa.

Wachapishaji

^ Kati ya habari ambazo zitapatikana tu kwenye Internete, kuna hizi zinazofuata: “Kwa Ajili ya Vijana,” habari ambayo inaonyesha miradi ya kujifunza Biblia ambayo vijana wanaweza kujiwekea, na “Ninajifunza Biblia,” mufululizo wa habari zilizotayarishwa kwa ajili ya wazazi ili kuzitumia wanapofundisha watoto wao wasiozidi miaka mitatu.