Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UWAFUNDISHE WATOTO WAKO

Mungu Anaweza Kuhuzunika—Namna Tunavyoweza Kumufurahisha

Mungu Anaweza Kuhuzunika—Namna Tunavyoweza Kumufurahisha

Je, umekwisha kuhuzunika sana hivi kwamba ukalia?​— * Inawezekana sisi wote tumekwisha kuhuzunika ao kuumizwa moyoni. Hata hivyo, wakati fulani, maumivu hayo si maumivu ya mwili. Mutu fulani anaweza kusema mambo mabaya yasiyo ya kweli juu yetu. Mambo hayo yanaweza kutuhuzunisha ao kutuumiza moyoni, sivyo?​— Mungu pia anaweza kuhuzunika wakati watu wanamusemea mambo yasiyo ya kweli. Acheni tuzungumuzie jambo hilo na tuone namna tunaweza kumufurahisha kuliko kumuhuzunisha.

Biblia inasema kwamba watu fulani ambao walisema kwamba wanamupenda Mungu, ‘walimuhuzunisha.’ Ndiyo, ‘walimutia uchungu’ Mungu! Kwa kweli, hakuna mutu anayeweza kuumiza mwili wa Yehova Mungu. Yeye ni mweza yote. Acheni tuone basi sababu gani Yehova anahuzunika ao kuumizwa moyoni wakati hatufanye mambo ambayo anasema.

Watu wawili wa kwanza ambao Yehova aliumba duniani walimuhuzunisha sana. Watu hao wawili waliwekwa katika Paradiso duniani inayoitwa “bustani ya Edeni.” Watu hao wawili ni nani?​— Ni Adamu, na Eva, aliyeumbwa baadaye. Acheni tuone jambo ambalo walifanya ambalo lilimuhuzunisha Yehova.

Kisha Yehova kuwatia katika bustani hiyo, aliwaambia waitunze. Pia aliwaambia kwamba wangezaa watoto na kuishi pamoja nao katika bustani hiyo bila kufa. Lakini mbele Adamu na Eva wazae watoto, jambo mbaya sana lilitokea. Unajua ni jambo gani?​— Malaika mumoja alimuchochea Eva na kisha Adamu kumuasi Yehova. Acheni tuone namna jambo hilo lilivyotokea.

Malaika huyo alifanya nyoka aonekane kuwa mwenye kusema. Eva alifurahia mambo ambayo alisikia​—nyoka alisema kwamba Eva angekuwa “kama Mungu.” Kwa hiyo, Eva alifanya kama nyoka alivyomuambia. Unajua alifanya nini?​—

Eva alikula tunda la muti ambao Yehova alimuambia Adamu kwamba hawakupaswa kula matunda yake. Mbele ya Mungu kuumba Eva, alimuambia Adamu hivi: ‘Matunda ya kila muti wa bustani unaweza kula mupaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.’

Eva alijua sheria hiyo. Lakini, aliendelea kuutazama muti huo, na akaona kwamba ‘ulikuwa muzuri kwa chakula na kwamba ulikuwa kitu cha kutamanika kwa macho . . . Kwa hiyo akaanza kuchukua kati ya matunda yake akakula.’ Kisha akamupatia Adamu tunda, naye “akaanza kula.” Unajua ni sababu gani Adamu alikula tunda hilo?​— Ni kwa sababu Adamu alimupenda Eva sana kuliko Yehova. Adamu alichagua kumufurahisha Eva kuliko kumufurahisha Mungu. Lakini kumutii Yehova ni jambo la maana sana kuliko kumutii mutu mwengine yeyote!

Je, unakumbuka nyoka ambaye alizungumuza na Eva? Kama vile mutu anavyoweza kufanya sanamu ao popi ionekane kuwa inasema, mutu fulani alifanya nyoka huyo aonekane kuwa ndiye mwenye kusema. Sauti iliyokuwa ikitoka kupitia nyoka ilikuwa ya nani?— Ilikuwa sauti ya “yule nyoka wa zamani, anayeitwa Ibilisi na Shetani.”

Unajua namna gani unaweza kumufurahisha Yehova?— Unaweza kufanya hivyo kwa kujaribu kumutii sikuzote. Shetani anasema kwamba anaweza kumufanya kila mutu atende mambo ambayo yeye anataka. Kwa hiyo, Yehova anatushauri hivi: ‘Uwe na hekima, mwanangu [ao binti yangu], na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipate kumujibu anayenizihaki.’ Shetani anamuzihaki ao kumucheka Yehova. Anasema kwamba anaweza kumufanya kila mutu aache kumutumikia Yehova. Kwa hiyo, umufurahishe Yehova kwa kuendelea kumutii na kumutumikia! Je, utajikaza kufanya hivyo?

^ Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii (—), utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.