Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | SABABU GANI MAMBO MABAYA YANAFIKIA WATU WAZURI?

Mambo Mungu Atafanya Juu ya Mabaya

Mambo Mungu Atafanya Juu ya Mabaya

Biblia inatueleza waziwazi mambo Yehova na Yesu Kristo, Mwana wake, watafanya juu ya mateso yenye kuletwa na Shetani Ibilisi. Biblia inasema hivi: “Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu [Yesu] alifunuliwa, yaani, ili azivunje kazi za Ibilisi.” (1 Yohana 3:8) Ulimwengu huu unaojaa pupa (ao tamaa mbaya), chuki, na matendo mabaya utaharibiwa. Na kuhusu ‘mutawala wa ulimwengu huu,’ ni kusema, Shetani Ibilisi, Yesu Kristo aliahidi kwamba ‘atatupwa inje.’ (Yohana 12:31) Bila ushawishi wa Shetani, ulimwengu mupya wa haki utasimamishwa, na dunia hii itakuwa mahali penye amani.—2 Petro 3:13.

Itakuwa namna gani juu ya wale wanaokataa kwa kiburi kubadilisha njia zao na wanaendelea kufanya mambo mabaya? Fikiria ahadi hii iliyo wazi: ‘Kwa maana wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake. Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani; nao wenye hila [ao wenye ujanja], watangolewa [ao kuondolewa] kutoka ndani yake.’ (Methali 2:21, 22) Ushawishi wa wanadamu waovu hautakuwa tena. Katika hali hizo zenye amani, wanadamu watiifu wataondolewa polepole katika hali ya kutokamilika yenye waliriti.—Waroma 6:17, 18; 8:21.

Katika dunia hiyo mupya, namna gani Mungu atamaliza mambo mabaya? Hatafanya hivyo kwa kukomesha zawadi ya uhuru wa kuchagua na kufanya watu watende kama roboti (ao mashine). Lakini, atafundisha wanadamu watiifu njia zake, na kuwasaidia waache mawazo na matendo yenye kuharibu.

Mungu ataondoa sababu zote zinazofanya kuwe mateso

Mungu atafanya nini juu ya misiba isiyotazamiwa? Ameahidi kwamba hivi karibuni serikali ya Ufalme wake itaongoza dunia. Mungu amemuweka Yesu Kristo kuwa Mufalme wa Ufalme huo, na Yesu iko na nguvu za kuponya magonjwa. (Mathayo 14:14) Pia, Yesu iko na uwezo wa kuzuia nguvu za asili. (Marko 4:35-41) Kwa hiyo, mateso yanayotokezwa na “wakati na tukio lisilotazamiwa” hayatakuwa tena. (Mhubiri 9:11) Katika utawala wa Kristo, hakuna musiba utakaopata wanadamu.—Methali 1:33.

Itakuwa namna gani juu ya mamilioni ya watu wasio na kosa wenye wamekufa katika misiba? Muda mufupi mbele ya kumufufua rafiki yake Lazaro, Yesu alisema hivi: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.” (Yohana 11:25) Kwa kweli, Yesu ana uwezo wa kufufua watu waliokufa, ao kuwarudisha kwenye uzima!

Ikiwa unapendezwa na wazo la kuishi katika dunia kwenye mambo mabaya hayatafikia watu wazuri, ufanye mupango wa kujifunza Biblia ili kujua mengi juu ya Mungu wa kweli na kusudi lake. Mashahidi wa Yehova wa eneo lako watafurahi kukusaidia ujifunze mambo hayo. Tunakualika kwa furaha uwatafute mahali unaishi ao uandikie wachapishaji wa gazeti hili.