Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUPATA FAIDA WAKATI UNASOMA BIBLIA?

Namna Gani Ninaweza Kuanza Kusoma Biblia?

Namna Gani Ninaweza Kuanza Kusoma Biblia?

Ni mambo gani yanaweza kukusaidia ufurahie kusoma Biblia na upate faida wakati unaisoma? Ona mambo tano yenye yamesaidia watu wengi.

Utafute mahali pa muzuri. Jaribu kutafuta mahali pa kimya. Ujikaze kuepuka mambo yenye yanaweza kukufanya usikazie akili yako juu ya mambo unasoma. Mwangaza muzuri na hewa ya muzuri vinaweza kukusaidia kupata faida wakati unasoma.

Ukuwe na mawazo ya muzuri. Kwa sababu Biblia inatoka kwa Baba yetu wa mbinguni, utapata faida zaidi ikiwa unakuwa kama mutoto mwenye iko tayari kujifunza kutoka kwa muzazi wake mwenye upendo. Kama uko na mawazo yoyote ya mubaya juu ya Biblia, jaribu kuyatia pembeni ili Mungu akufundishe.​—Zaburi 25:4.

Usali mbele ya kuanza kusoma. Biblia iko na mawazo ya Mungu, ndiyo sababu tuko na lazima ya musaada wake ili kuielewa. Mungu anaahidi kuwapatia “roho takatifu wale wanaomwomba.” (Luka 11:13) Roho takatifu inaweza kukusaidia kuelewa mawazo ya Mungu. Kisha wakati fulani, itafungua akili yako ili uweze kuelewa “hata mambo mazito ya Mungu.”—1 Wakorintho 2:10.

Ujikaze kuelewa mambo unasoma. Hapana kusoma juu tu ya kumaliza Biblia. Fikiria sana juu ya mambo yenye unasoma. Kwa mufano, unaweza kujiuliza hivi wakati unasoma habari juu ya mutu fulani: ‘Mutu huyu alionyesha sifa gani? Namna gani ninaweza kutumia habari hii katika maisha yangu?’

Upange mambo yenye unapenda kutimiza. Ili upate faida wakati unasoma Biblia, ujikaze kujifunza jambo fulani lenye litakusaidia kabisa katika maisha yako. Unaweza kupanga kutimiza mambo kama haya: ‘Ninataka kujifunza mengi zaidi juu ya Mungu.’ ‘Ninapenda kuwa mutu muzuri zaidi, bibi ao bwana muzuri zaidi.’ Kisha chagua Maandiko ya Biblia yenye yatakusaidia kutimiza mambo hayo. *

Mambo hayo tano yatakusaidia kuanza kusoma Biblia. Lakini unaweza kufanya nini ili ufurahie zaidi kusoma Biblia? Habari yenye kufuata inaonyesha mambo fulani ya kufanya.

^ fu. 8 Kama haujue muzuri ni Maandiko gani ya Biblia yenye yatakusaidia zaidi kufikia mambo yenye unapenda kutimiza, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia.