KUANZISHA MAZUNGUMUZO
SOMO YA 1
Kupendezwa na Watu
Kanuni: “Upendo . . . hautafute faida zake wenyewe.”—1 Ko. 13:4, 5.
Mambo Yenye Yesu Alifanya
1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 4:6-9. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:
Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?
2. Mazungumzo yetu itakuwa ya muzuri kama tunaanza na habari yenye inafurahisha musikilizaji.
Umuige Yesu
3. Ujipatanishe na hali. Usianze mazungumzo vile tu weye ulipanga mu akili. Uanze na habari ya sasa yenye wengine wako wanafikiria. Ujiulize hivi:
4. Ukuwe muangalifu. Ujiulize hivi:
-
‘Namna alishavala, namna anaonekana, na pia nyumba yake vinaonyesha nini juu ya imani yake na desturi yake?’
5. Usikilize.
-
Umusaidie mwenye uko naongea naye ajisikie huru kusema mawazo yake. Kama ni muzuri umuulize maulizo.