Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 2

Rebeka Alipenda Kumufurahisha Yehova Sana

Rebeka Alipenda Kumufurahisha Yehova Sana

Rebeka alikuwa anamupenda Yehova sana. Bwana yake anaitwa Isaka. Isaka pia alimupenda Yehova. Namna gani Isaka alifikia kumuoa Rebeka? Namna gani Rebeka alionyesha kama anapenda kumufurahisha Yehova sana? Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya mwanamuke huyo Rebeka.

Abrahamu ndiye alikuwa baba ya Isaka, na Sara alikuwa mama yake. Familia hiyo iliishi katika inchi ya Kanaani. Watu wa Kanaani hawakuwa wanamuabudu Yehova. Lakini, Abrahamu alipenda mutoto wake aoe mwanamuke mwenye kumuabudu Yehova. Basi, Abrahamu alimutuma mutumishi wake amutafutie Isaka mwanamuke kule Harani. Inaonekana alimutuma Eliezeri. Watu fulani wa jamaa ya Abrahamu walikuwa wanaishi kule Harani.

Rebeka alifurahia kutumika sana ili kuletea ngamia maji ya kunywa

Eliezeri alifanya safari ya kuenda Harani pamoja na watumishi wengine wa Abrahamu. Walifanya safari murefu sana. Walienda na ngamia kumi zenye kubeba chakula na zawadi mbalimbali. Namna gani Eliezeri angejua mwanamuke wa kumuchagulia Isaka? Wakati Eliezeri na watumishi wenzake wanafika Harani, wanapumuzika ku kisima cha maji. Wanapumuzika pale juu Eliezeri anajua kama wanawake wa Harani wako karibu kuja kushota maji. Anasali kwa Yehova hivi: ‘Mutoto mwanamuke mwenye nitaomba maji, na akinipatia miye na ngamia zangu maji ya kunywa, basi nitajua kama huyo ndiye mwanamuke mwenye umechagulia mutumishi wako.’

Kisha Rebeka anafika ku kisima cha maji. Biblia inasema kama alikuwa na sura yenye kupendeza sana. Eliezeri anamuomba Rebeka maji ya kunywa, na Rebeka anamuambia hivi: ‘Nitakupatia maji, na ukisha kunywa, nitaenda kuletea pia ngamia zako maji.’ Lakini waza kidogo! Ngamia wenye kuwa na kiu wanakunywa maji mingi sana. Kwa hiyo, inamuomba Rebeka akimbie na kuenda tena na tena ku kisima cha maji ili kuletea ngamia maji. Angalia picha hii. Unaona vile Rebeka anatumika sana?— Eliezeri anashangaa sana kuona vile Yehova anajibia sala yake.

Eliezeri anamupatia Rebeka zawadi nyingi zenye kupendeza sana. Kisha Rebeka anamuambia Eliezeri na watumishi wenzake waende pamoja ku nyumba ya wazazi wake. Wakati walifika, Eliezeri akaanza kuwaelezea wazazi wa Rebeka juu ya nini Abrahamu alimutuma, na vile Yehova amejibia sala yake. Wazazi wa Rebeka na ndugu zake wakafurahi sana na wakaitika Rebeka aolewe na Isaka.

Rebeka anaenda Kanaani na Eliezeri ili kuolewa na Isaka

Unawaza Rebeka aliitika kabisa kuolewa na Isaka?— Rebeka aliitika kwa sababu alijua kama Yehova ndiye alimutuma Eliezeri. Kwa hiyo, wakati wazazi wa Rebeka na ndugu zake wanamuuliza kama anapenda kuenda Kanaani ili akuwe bibi ya Isaka, Rebeka anajibu hivi: ‘Ndiyo, ninapenda kuenda.’ Mara moja anaenda na Eliezeri. Wakati wanafika Kanaani, Isaka anamuoa Rebeka.

Rebeka alifanya mambo yenye Yehova alipenda afanye. Kwa hiyo, Yehova alimusaidia. Kisha miaka mingi, Yesu alizaliwa katika familia ya Rebeka! Ukifuata mufano wa Rebeka kwa kumufurahisha Yehova sana, wewe pia Yehova atakusaidia.

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO